Download - islamic education panel
Download - islamic education panel
Download - islamic education panel
Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
Nu’man bin Bashir (r.a) amesema kuwa Mtume wa Allah<br />
amesema: “utawaona waumini wakifanyiana wema,<br />
wakipendana na kuhurumiana kama mwili mmoja. Wakati<br />
kiungo kimoja kikiugua, mwili mzima huhisi homa na<br />
hukesha (kwa maumivu). (Bukhari na Muslim)<br />
Aidha katika Hadith nyingine,<br />
Nu’uman bin Bashir (r.a) amesema kuwa Mtume wa Allah<br />
amesema: “Waumini ni sawa na mwili mmoja. Kama<br />
macho yanauma (yana matatizo), mwili mzima unauma<br />
(una matatizo), kama kichwa chake kinauma basi mwili<br />
mzima unauma”. (Muslim).<br />
Hadith hizi zinatufahamisha na kutukumbusha kuwa tatizo<br />
la Muislam mmoja ni tatizo la Waislamu wote, kwa hiyo hawana<br />
budi kushirikiana pamoja kwa hali na mali katika kuondoa tatizo<br />
hilo.<br />
(ii) Kutekelezeana wajibu<br />
Kila Muislamu anawajibika kumtendea Muislamu mwenziwe<br />
mambo sita yaliyoelezwa katika Hadith ifuatayo:<br />
Abu Hurairah (r.a) ameeleza kuwa Mtume wa Allah<br />
amesema: Haki za Muislamu kwa Muislamu mwingine ni<br />
sita. Ikaulizwa ni zipi hizo ewe Mtume wa Allah? Akajibu:<br />
(1) Ukikutana naye msalimie; (2) Akikuita mwitikie; (3)<br />
Akitaka ushauri mpe; (4) Akipiga chafya na akasema Alhamdulillah<br />
mwitikie (mrehemu kwa kusema<br />
Rahmakallaah); (5) Anapokuwa mgonjwa, nenda<br />
kamtazame na (6) Anapokufa fuata jeneza lake (mzike).<br />
(Muslim)<br />
89