08.06.2013 Views

Download - islamic education panel

Download - islamic education panel

Download - islamic education panel

SHOW MORE
SHOW LESS

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

Uongozi wa Kitwaghuti husimamia batili na dhulma na<br />

matokeo yake ni kuenea ufisadi katika ardhi. Uongozi wa<br />

kitwaghuti hufanya ufisadi huku ukijitangaza kuwa unasimamia<br />

amani, usalama na maendeleo ya watu. Tabia hii ya uongozi wa<br />

Kitwaghuti Allah (s.w) anaiweka wazi katika aya zifuatazo:<br />

Na wanapoambiwa: “Msifanye uharibifu ulimwenguni” Husema<br />

“Sisi ni watengezaji.”(2:11)<br />

Hakika wao ndio waharibifu, lakini hawatambui. (2:12)<br />

Sifa za kiongozi wa kiislamu<br />

Katika Uislamu kiongozi hachaguliwi kwa kufanya kampeni<br />

ya kuomba kura kwa mujibu wa Hadith zifuatazo:<br />

"Abdul-Rahmaan bin Sanurah(r.a) amesimulia kuwa Mtume wa<br />

Allah amesema: usiombe uongozi kwa sababu utakapo pewa<br />

uongozi kwa kuomba utaachiwa peke yako jukumu la uongozi, na<br />

kama umepewa bila kuomba utasaidiwa katika uongozi huo."<br />

(Bukhari na Muslim)<br />

Katika Hadith nyingine aliyosimulia Abu Mussa, Mtume<br />

(s.a.w) amesema:-<br />

"Hatumchagui kwenye uongozi huu yeyote anayeomba wala<br />

hachaguliwi yule aliyemroho wa uongozi". (Bukhari na Muslim)<br />

Katika Uislamu mtu huwa kiongozi kwa kuchaguliwa na watu<br />

na kubebeshwa jukumu hili kwa ajili ya Allah:<br />

190

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!