Download - islamic education panel
Download - islamic education panel
Download - islamic education panel
Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
haikuweka mipango inayoonesha inataka ifikie malengo gani<br />
katika kipindi cha miaka mitano ijayo, ni wazi kuwa miaka hiyo<br />
mitano itapita bila ya kufanyika lolote na bila kuhisi vibaya<br />
kwamba hakuna mafanikio yaliyopatikana, kwani tangu hapo<br />
hapakuwa na malengo ya kufanya lolote. Lakini jaalia kwa mfano,<br />
waumini wa msikiti wa Mwanza Mabatini wanampango wa kuwa<br />
na (a) Shule safi ya awali, (b) Zahanati yenye kuendeshwa kwa<br />
maadili ya Kiislamu na (c) Mfuko wa fedha wa kuwasaidia vijana<br />
na akina mama wa Kiislamu kuanzisha biashara ndogo ndogo<br />
katika kipindi cha miaka mitano. Ni lazima viongozi na waumini<br />
watahangaika kuhakikisha malengo hayo yanafikiwa. Kwa kuwa<br />
na mpango huu zitapatikana faida zifuatazo:<br />
(i) Waumini watakuwa na kigezo cha kupima utendaji wa<br />
viongozi wao kama wanafaa au laa.<br />
(ii) Waumini hawatapoteza muda wao, nguvu na mali zao<br />
katika mambo yasiyowapelekea kwenye lengo na watajua<br />
nguvu na uwezo wao kuliko kubakia kila siku katika<br />
nadharia.<br />
(iii)Aidha, ni katika utekelezaji wa malengo yaliyowekwa<br />
watafahamika Waislamu wa kweli (watekelezaji) na wale<br />
washabiki tu wa kupiga takbira zisizo na utendaji.<br />
Aina ya mipango<br />
(1) Mipango ya muda mfupi<br />
- Utekelezaji wake huchukua mwaka 1 -3<br />
- Utekelezaji wake pia huchangia kufikia malengo ya mpango<br />
wa muda mrefu.<br />
(2) Mipango ya muda mrefu:<br />
- Utekelezaji wake huchukua zaidi ya miaka 3<br />
- Hugawanywa katika mipango ya muda mfupi mfupi<br />
171