08.06.2013 Views

Download - islamic education panel

Download - islamic education panel

Download - islamic education panel

SHOW MORE
SHOW LESS

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

(i) Kuliweka Bayana Lengo la Elimu.<br />

Mwalimu kabla hajaanza kufundisha somo lake ni muhimu<br />

kwanza awaweke sawa wanafunzi wake juu ya nafasi na lengo la<br />

elimu katika Uislamu. Ukizingatia historia iliyobainishwa katika<br />

Qur’an elimu imechukua nafasi mbili zifuatazo:<br />

(1) Takrima ya kwanza aliyotunukiwa binaadamu na Mola<br />

wake.<br />

Neema ya kwanza aliyotunukiwa Adam (a.s) baada tu ya<br />

kuumbwa kwake ni kuelimishwa na Mola wake.<br />

.................<br />

“Na Mwenyezi Mungu akamfundisha Adam Majina ya vitu vyote<br />

…” (2:30).<br />

“Majina ya vitu vyote” katika aya hii inaashiria fani zote<br />

za elimu ya mazingira ambazo anahitajia mwanaadamu hapa<br />

ulimwenguni. Kisha Adam (a.s) na mkewe Hawwah<br />

waliposhushwa kuanza maisha ya Ukhalifa hapa duniani<br />

waliahidiwa elimu ya Mwongozo.<br />

Tukasema; “Shukeni humo nyote; na kama ukikufikieni uwongozi<br />

utokao Kwangu, basi watakaofuata uwongozi Wangu huo<br />

haitakuwa khofu juu yao wala hawatahuzunika” (2:38).<br />

(2) Amri ya kwanza aliyopewa Mtume (s.a.w) na kwahiyo<br />

watu wote wa Ummah wake ni kutafuta Elimu:-<br />

211

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!