Download - islamic education panel
Download - islamic education panel
Download - islamic education panel
Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
Katika hali halisi ni vigumu kupatikana umma wa Kiislamu<br />
kutokana na jamii ya kijahili pasi na maandalizi. Uwezekano wa<br />
kuunda umma huo utakaosimamisha Uislamu katika jamii<br />
utakuwepo tu pale Waislamu wachache watakapotanabahi na<br />
kuunda kundi lililoshikamana barabara likajizatiti katika<br />
kulingania Uislamu, kuamrisha mema na kukataza<br />
maovu katika jamii kama alivyojizatiti Mtume (s.a.w) na<br />
maswahaba wake. Kuhusu kundi hili Allah (s.w) anaagiza:<br />
“Na wawepo katika nyinyi watu wanaolingania kheri<br />
(Uislamu) na wanaoamrisha mema na kukataza maovu na<br />
hao ndio watakaotengenekewa.” (3:104).<br />
Sifa za kundi la harakati<br />
Si kila kundi litakalojitokeza na kudai kuwa linalingania<br />
Uislamu katika jamii litakuwa lile lililoagizwa katika Qur-an<br />
(3:104). Vikundi vingi tunavyovifahamu vilivyojitangazia kuwa ni<br />
vikundi vya Harakati vimeishia katika kuwafarakanisha Waislamu<br />
na kuzidi kuwapa mwanya maadui wa Uislamu wazidi<br />
kuuangamiza. Tukumbuke kuwa kazi hii ni kazi takatifu<br />
iliyofanywa na Mitume wa Allah (s.w) na wale walioamini pamoja<br />
nao. Hivyo, mafanikio katika kazi hii yatapatikana tu kama kundi<br />
la Harakati litaigiza vilivyo mwenendo wa Mitume na walioamini<br />
pamoja nao katika kufanya kazi hii.<br />
Kundi la Harakati ili liweze kufanikiwa katika kuhuisha<br />
Uislamu na kuusimamisha katika jamii linalazimika kwa ujumla<br />
wake liwe na sifa za msingi zifuatazo:<br />
83