08.06.2013 Views

Download - islamic education panel

Download - islamic education panel

Download - islamic education panel

SHOW MORE
SHOW LESS

You also want an ePaper? Increase the reach of your titles

YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.

Kwa nini ni muhimu kusimamisha Uislamu katika<br />

Jamii ?<br />

Kusimamisha Uislamu kumefaradhishwa kwa waumini ili<br />

yapatikane yafuatayo:<br />

(i) Waumini waweze kumuabudu Allah (s.w) ipasavyo.<br />

(ii) Kuleta amani ya kweli katika jamii.<br />

(iii) Waumini waweze kuamrisha mema na kukataza maovu.<br />

(iv) Kuikinga jamii na majanga mbali mbali.<br />

(i) Waumini kuweza kumuabudu Mola wao<br />

ipasavyo<br />

Allah (s.w.) amewaumba majini na watu kwa lengo moja tu la<br />

kumuabudu<br />

“Sikuwaumba majini na watu ila wapate kuniabudu.” (51:56)<br />

Kumuabudu Allah (s.w.) kwa mnasaba wa lengo la kuumbwa<br />

watu, ni watu kuishi katika kila kipengele cha maisha yao kwa<br />

kufuata baraabara kanuni, sharia na mwongozo wa Allah (s.w.).<br />

Kimantiki Allah (s.w) ndiye pekee anayestahiki kuabudiwa au<br />

kutiiwa na binaadamu kwa unyenyekevu katika kukiendea kila<br />

kipengele cha maisha yake ya kibinafsi na kijamii kwa kuwa yeye<br />

ndiye aliyemuumba binaadamu na maumbile yote yaliyomzunguka<br />

pamoja na kumtunukia neema mbali mbali kama tunavyojifunza<br />

katika aya zifuatazo:<br />

14

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!