08.06.2013 Views

Download - islamic education panel

Download - islamic education panel

Download - islamic education panel

SHOW MORE
SHOW LESS

You also want an ePaper? Increase the reach of your titles

YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.

linapoteleza na kwenda nje ya lengo. Kundi linaweza kujikuta<br />

halipati matunda yaliyokusudiwa pamoja na nia yake safi, lengo<br />

sahihi na muelekeo sahihi wa kuliendea lengo, kutokana na<br />

makosa yaliyojiingiza bila ya kung’amuliwa na kurekebishwa.<br />

Hivyo ili kundi la Harakati liepukane na makosa yanayojipenyeza<br />

mara kwa mara katika harakati, halina budi kuwa na utaratibu<br />

maalumu wa kukosoana kwa mwanakundi mmoja mmoja na kundi<br />

lote kwa ujumla.<br />

Katika kukosoana inatakiwa kuchukua tahadhari kubwa,<br />

kwani endapo patafanyika kosa katika kufanya kazi hii,<br />

inawezekana ikawa ni sababu ya kuharibu zaidi kuliko<br />

kutengeneza. Kukosoa kuepukane kabisa na sura ya<br />

kudhalilishana, kudharauliana, kulaumiana, kuvunjiana heshima,<br />

n.k. Kukosoana kuwe kwa nia ya kumrejesha mwanakundi au<br />

kundi lote kwenye njia sahihi ya kuliendea lengo baada ya<br />

kuridhika kuwa mwana kundi au kundi kwa ujumla, linakwenda<br />

kinyume kidogo na lengo. Mkosoaji hana budi kuonesha huruma<br />

na upendo kwa huyo anayemkosoa na hana budi kutumia lugha<br />

nzuri na hekima kubwa katika kumkosoa. Mkosoaji mwenye nia<br />

nzuri kabisa, asiyetumia lugha nzuri na hekima, huweza kuingiza<br />

doa jeusi katika kundi na kudhoofisha mshikamano wa kundi na<br />

hatimaye kulifarakanisha. Pamoja na nia yake njema, mkosoaji<br />

huyu asiyetumia hekima na lugha nzuri katika kukosoa, hana<br />

tofauti na wale wanao wakosoa wenzao kwa kuwazulia makosa ili<br />

tu wawadhalilishe na kuwavunjia hadhi na heshima yao ili wao<br />

waonekane kuwa ndio bora na wanaofaa zaidi.<br />

Kwa upande mwingine mwenye kukosolewa kwa nia njema<br />

na kwa utaratibu unaotakikana awetayari kukosolewa na<br />

kujirekebisha kwa moyo mkunjufu. Mwenye kukosolewa kwa nia<br />

njema hana budi kuona kuwa amefanyiwa ihsani na mkosoaji kwa<br />

kumrudisha katika njia sahihi ya kuendea lengo. Mkosolewaji<br />

anatakiwa amuone ndugu yake anayemkosoa kama kioo ambacho<br />

103

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!