08.06.2013 Views

Download - islamic education panel

Download - islamic education panel

Download - islamic education panel

SHOW MORE
SHOW LESS

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

Hakika sisi tutakuteremshia kauli nzito. Hakika kuamka usiku<br />

kunawafikiana zaidi na moyo na maneno yake yanatuwa zaidi.<br />

Hakika mchana unashughuli nyingi. Na litaje jina la Mola wako<br />

na ujitupe kwake kwa kweli. (73:5-8)<br />

(Yeye Ndiye)Mola wa mashariki na magharib, Hapana<br />

Mola ila yeye, basi mfanye kuwa mlinzi wako. Na subiri juu<br />

ya hayo wayasemayo na uwaepuke mwepuko mwema.”<br />

(73:9-10)<br />

Aya ya kwanza ya sura hii inaashiria kuwa huu ni wahyi wa<br />

mwanzo mwanzo uliofuatia wahyi wa kwanza. Katika Hadith<br />

iliyosimuliwa na Bibi Aysha (r.a), tunafahamishwa kuwa Mtume<br />

(s.a.w) alistushwa sana na lile tukio la Pangoni Hira, la<br />

kulazimishwa kusoma na Malaika Jibril ambaye ilikuwa ni mara<br />

yake ya kwanza kukutana naye. Mtume(s.a.w) alirudi nyumbani<br />

akiwa anatetemeka kama mtu mwenye homa kali. Alimuomba<br />

mkewe Khadija amfunike nguo. Baada ya muda hali ile ya khofu<br />

iliisha na kuweza kumhadithia mkewe yale yaliyomtokea.<br />

Alipomuona tena Jibril (a.s) anamjia kumletea wahay uliomo<br />

mwanzoni mwa sura hii (73:1-10) Mtume (s.a.w) alistuka tena na<br />

kujaribu kujihami asijefikwa na yale yaliyo mfika pangoni kwa<br />

kujifunika tena nguo. Lakini bado Jibril alimuendea Mtume<br />

(s.a.w) katika hali ile ile ya kujifunika na kumfikishia ujumbe huu<br />

wenye kumuamrisha kufanya yafuatayo:<br />

51

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!