08.06.2013 Views

Download - islamic education panel

Download - islamic education panel

Download - islamic education panel

SHOW MORE
SHOW LESS

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

Tumeeleza awali kuwa Mtume (s.a.w) aliondoka Madinah<br />

kwenda Makkah kufanya Umra, lakini Maquraish wakamzuia.<br />

Kufanya Umra japo ni Ibada lakini haikuwa ndio jambo la<br />

kistratejia la kuufanya Uislamu usimame, kwa kujua hilo Mtume<br />

(s.a.w) alikuwa tayari kuikosa Umra hiyo lakini ajenge mazingira<br />

ya kumwezesha kuufikisha ujumbe wa Uislamu kwa watu.<br />

Je, ni wangapi miongoni mwetu, wenye mtizamo huo?<br />

Hatufarikiani katika Misikiti na taasisi kwa tofauti ndogo tu<br />

ambazo tangu hapo hazina msaada wowote katika kulifikia lengo?<br />

Jumuiya ngapi zimesambaratika kutokana na migogoro isiyokuwa<br />

na msingi?<br />

Uoni na Mwelekeo (Vision na Direction)<br />

Katika kuweka mipango, ni lazima kwanza mtu ajue<br />

analolenga kufikia na njia anayokusudia kupita. Tunakolenga<br />

Waislamu ni kusimamisha Uislamu katika jamii. Mwelekeo na njia<br />

tunayopita ni ile ya kuwaelimisha Waislamu wakaijua na kuifuata<br />

Qur-an katika kila kipengele cha maisha yao. Darasa za Misikitini<br />

zinazoratibiwa vizuri, madrasa za watoto na watu Wazima, shule za<br />

msingi na sekondari za Kiislamu, uchapishaji na usambazaji wa<br />

vitabu na kadhalika ni katika njia za kutupeleka tunakokusudia<br />

kufika. Aidha programu kama kuandaa mihadhara, semina,<br />

itikafu, na kuanzisha taasisi za Kiislamu za kushughulikia mambo<br />

mbali mbali ni miongoni pia mwa njia za kuendea kwenye lengo.<br />

Kuwa na uoni huu ni muhimu kwani wakati mwingine watu<br />

waweza kufanikiwa kuwa na vitu kama shule safi za watoto<br />

(Chekechea) au sekondari za Kiislamu wakidhani ndio wamefika.<br />

Akili zao na juhudi zao zote zikaishia kuziangalia shule hizo,<br />

wasiwe na mpango mwingine wa kusonga mbele. Au watu waweza<br />

kuwa na utaratuibu wao mzuri wa kutoa mihadhara, kuendesha<br />

Itikafu na kadhalika wakaona imetosha. Na madhali hawazuiliwi<br />

na mamlaka yoyote kufanya shughuli hizo wakatosheka, bila<br />

kufikiria kwamba:<br />

184

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!