Download - islamic education panel
Download - islamic education panel
Download - islamic education panel
Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
Tumeeleza awali kuwa Mtume (s.a.w) aliondoka Madinah<br />
kwenda Makkah kufanya Umra, lakini Maquraish wakamzuia.<br />
Kufanya Umra japo ni Ibada lakini haikuwa ndio jambo la<br />
kistratejia la kuufanya Uislamu usimame, kwa kujua hilo Mtume<br />
(s.a.w) alikuwa tayari kuikosa Umra hiyo lakini ajenge mazingira<br />
ya kumwezesha kuufikisha ujumbe wa Uislamu kwa watu.<br />
Je, ni wangapi miongoni mwetu, wenye mtizamo huo?<br />
Hatufarikiani katika Misikiti na taasisi kwa tofauti ndogo tu<br />
ambazo tangu hapo hazina msaada wowote katika kulifikia lengo?<br />
Jumuiya ngapi zimesambaratika kutokana na migogoro isiyokuwa<br />
na msingi?<br />
Uoni na Mwelekeo (Vision na Direction)<br />
Katika kuweka mipango, ni lazima kwanza mtu ajue<br />
analolenga kufikia na njia anayokusudia kupita. Tunakolenga<br />
Waislamu ni kusimamisha Uislamu katika jamii. Mwelekeo na njia<br />
tunayopita ni ile ya kuwaelimisha Waislamu wakaijua na kuifuata<br />
Qur-an katika kila kipengele cha maisha yao. Darasa za Misikitini<br />
zinazoratibiwa vizuri, madrasa za watoto na watu Wazima, shule za<br />
msingi na sekondari za Kiislamu, uchapishaji na usambazaji wa<br />
vitabu na kadhalika ni katika njia za kutupeleka tunakokusudia<br />
kufika. Aidha programu kama kuandaa mihadhara, semina,<br />
itikafu, na kuanzisha taasisi za Kiislamu za kushughulikia mambo<br />
mbali mbali ni miongoni pia mwa njia za kuendea kwenye lengo.<br />
Kuwa na uoni huu ni muhimu kwani wakati mwingine watu<br />
waweza kufanikiwa kuwa na vitu kama shule safi za watoto<br />
(Chekechea) au sekondari za Kiislamu wakidhani ndio wamefika.<br />
Akili zao na juhudi zao zote zikaishia kuziangalia shule hizo,<br />
wasiwe na mpango mwingine wa kusonga mbele. Au watu waweza<br />
kuwa na utaratuibu wao mzuri wa kutoa mihadhara, kuendesha<br />
Itikafu na kadhalika wakaona imetosha. Na madhali hawazuiliwi<br />
na mamlaka yoyote kufanya shughuli hizo wakatosheka, bila<br />
kufikiria kwamba:<br />
184