08.06.2013 Views

Download - islamic education panel

Download - islamic education panel

Download - islamic education panel

SHOW MORE
SHOW LESS

You also want an ePaper? Increase the reach of your titles

YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.

Faida za kushauriana<br />

Kuna faida nyingi zinazopatikana kutokana na kushauriana<br />

kwa kila uamuzi unaohusu shughuli za kundi la Harakati na faida<br />

mbili zifuatazo ziko wazi:<br />

Kwanza, kushauriana hutoa fursa kwa kila mwanakundi<br />

kutoa mawazo yake juu ya uendeshaji wa shughuli za Da’wah.<br />

Mchango wa mawazo kutoka kwa kila mwanakundi kutauwezesha<br />

uamuzi juu ya utekelezaji wa jambo, uwe ni wa hakika zaidi. Kwani<br />

kila mtu ana kipaji chake ambacho hakipo kwa mwingine - akili ni<br />

nywele kila mmoja ana zake.<br />

Pili, kwa kumpa kila mwanakundi nafasi ya kutoa ushauri<br />

wake juu ya jambo, uamuzi utakao fikiwa utakuwa ni wa kundi na<br />

kila mwanakundi atakuwa tayari kutekeleza kwa moyo mkunjufu<br />

maamuzi yaliyofikiwa. Hata utekelezaji ukiwa mgumu kiasi gani,<br />

hakuna atakayeona kuwa amepachikwa jukumu asiloafikiana nalo.<br />

Bali kila mwanakundi ataifanya shughuli yoyote atakayopewa mpaka<br />

aione hatima yake.<br />

Masharti ya kushauriana<br />

Katika kushauriana yafuatayo ni muhimu yazingatiwe.<br />

Kwanza, kila mmoja anatakiwa awe huru kutoa maoni yake juu<br />

ya jambo linalojadiliwa bila ya kusita wala kuficha chochote. Mawazo<br />

yake yasiathiriwe na upendeleo wala chuki.<br />

Pili, baada ya uamuzi kutolewa kutokana na kuzingatia mawazo<br />

ya kila mtu wale waliokuwa na maoni tofauti na uamuzi uliotolewa<br />

unaotokana na maoni ya wengi, hawana budi kwa moyo mkunjufu<br />

kukubaliana na uamuzi wa wengi hata kama hawajabadilisha mawazo<br />

yao.<br />

Tatu, uamuzi au maoni ya wengi hayataangaliwa kama<br />

yamekiuka Qur’an na Sunnah.<br />

101

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!