Download - islamic education panel
Download - islamic education panel
Download - islamic education panel
You also want an ePaper? Increase the reach of your titles
YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.
Faida za kushauriana<br />
Kuna faida nyingi zinazopatikana kutokana na kushauriana<br />
kwa kila uamuzi unaohusu shughuli za kundi la Harakati na faida<br />
mbili zifuatazo ziko wazi:<br />
Kwanza, kushauriana hutoa fursa kwa kila mwanakundi<br />
kutoa mawazo yake juu ya uendeshaji wa shughuli za Da’wah.<br />
Mchango wa mawazo kutoka kwa kila mwanakundi kutauwezesha<br />
uamuzi juu ya utekelezaji wa jambo, uwe ni wa hakika zaidi. Kwani<br />
kila mtu ana kipaji chake ambacho hakipo kwa mwingine - akili ni<br />
nywele kila mmoja ana zake.<br />
Pili, kwa kumpa kila mwanakundi nafasi ya kutoa ushauri<br />
wake juu ya jambo, uamuzi utakao fikiwa utakuwa ni wa kundi na<br />
kila mwanakundi atakuwa tayari kutekeleza kwa moyo mkunjufu<br />
maamuzi yaliyofikiwa. Hata utekelezaji ukiwa mgumu kiasi gani,<br />
hakuna atakayeona kuwa amepachikwa jukumu asiloafikiana nalo.<br />
Bali kila mwanakundi ataifanya shughuli yoyote atakayopewa mpaka<br />
aione hatima yake.<br />
Masharti ya kushauriana<br />
Katika kushauriana yafuatayo ni muhimu yazingatiwe.<br />
Kwanza, kila mmoja anatakiwa awe huru kutoa maoni yake juu<br />
ya jambo linalojadiliwa bila ya kusita wala kuficha chochote. Mawazo<br />
yake yasiathiriwe na upendeleo wala chuki.<br />
Pili, baada ya uamuzi kutolewa kutokana na kuzingatia mawazo<br />
ya kila mtu wale waliokuwa na maoni tofauti na uamuzi uliotolewa<br />
unaotokana na maoni ya wengi, hawana budi kwa moyo mkunjufu<br />
kukubaliana na uamuzi wa wengi hata kama hawajabadilisha mawazo<br />
yao.<br />
Tatu, uamuzi au maoni ya wengi hayataangaliwa kama<br />
yamekiuka Qur’an na Sunnah.<br />
101