Download - islamic education panel
Download - islamic education panel
Download - islamic education panel
Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
Ikumbukwe kuwa mwaka 1990 Padre mmoja wa Kanisa<br />
Katoliki aliomba Bakwata imruhusu awasomeshe watoto wa<br />
madrasa Qur’an na lugha ya Kiaarabu, ili waweze kusoma kwa<br />
muda mfupi kabisa. Bakwata walikataa. Kwa sababu watoto wa<br />
Kiislamu hawawezi kufundishwa dini yao na mtu anayeichukia na<br />
kuipiga vita dini hiyo.<br />
Leo, yale yale waliyoyakataa Bakwata wakati ule yanafanyika<br />
tena kwa shangwe na vifijo. Swali: Hivi kwanini leo Wamarekani<br />
wanaowauwa Waislamu wenzetu huko Afghanistan, Iraq na<br />
Palestina wakawa ndio wafadhili pekee wa madrasa huko Zanzibar<br />
kwenye asilimia 99 ya Waislamu? Kwanini makafiri hawa<br />
wanafanikiwa? Al-jawab. “Wamefuata zile kanuni za maadili<br />
ya kibinadamu” tulizozitaja hapo juu. Watu hawawezi kuijua na<br />
kuifuata Qur’an kwa sababu tu sisi tunatamani, na ilhali hatupo<br />
tayari kutumia mali zetu, nafsi zetu, wakati wetu na juhudi zetu<br />
kuhakikisha hilo linafanyika. Huko Zanzibar, USAID<br />
imekwishatumia mamilioni ya shilingi ili kufikia malengo yake.<br />
(ii) Maadili ya Kiislamu<br />
Maadili ya Kiislamu ni yale yale ya kibinaadamu isipokuwa<br />
kinachobadilika ni mwelekeo na matumizi ya maadili hayo.<br />
Maadili ya kibinaadamu yanapoongozwa na Tawhiid na yakawa<br />
lengo lake wakati wote ni kupata radhi za Allah (s.w) basi yatakuwa<br />
ni maadili ya Kiislamu. Maadili ya Kiislamu yanakuwa ni bora zaidi<br />
kwa sababu wakati wote yanatumika katika kusimamisha uadilifu<br />
katika jamii.<br />
Kanuni ya Allah kuhusu uongozi katika jamii<br />
Kanuni aliyoiweka Allah (s.w) kuhusu nani wawe viongozi<br />
katika jamii ni hii:<br />
Uongozi wa watu katika jamii siku zote huchukuliwa na wale<br />
watu ambao wamechanganya maadili ya kibinadamu na yale ya<br />
Kiislamu. lkiwa hakuna wenye sifa hiyo basi uongozi utakwenda<br />
kwa wale wenye maadili ya kibinaadamu, hata kama hawatakuwa<br />
34