Download - islamic education panel
Download - islamic education panel
Download - islamic education panel
Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
kumkashifu maiti huyo eti wanatoa heshima za mwisho! Hapana<br />
shaka yote hayo wamewaiga wakristo.<br />
Imefikia hadi mwezi wa Ramadhani badala ya Muislamu<br />
kumfuturisha Muislamu mwenzake kama alivyosisitiza sana<br />
Mtume (s.a.w) huwafuturisha wakristo ambao hawakufunga kana<br />
kwamba hakuna Waislamu waliofunga.<br />
Na katika kuhakikisha kuwa tunawafuata wakristo katika<br />
kila jambo, yupo Muislamu mmoja tena Al-haj, akafikia hadi<br />
kujipa jukumu la kuandaa karamu ya kusherehekea Noeli na yeye<br />
ndiye aliyewaalika Wakristo waende kula sikukuu! Kwa sababu ni<br />
kiongozi maarufu, picha yake ikawekwa ukurasa wa mbele wa<br />
gazeti la Sunday News! Hayo ni mafanikio ya maadui ambao<br />
Waislamu wamehadharishwa nao lakini hawasikii.<br />
Mfano mwingine wa mikakati yao tunauona katika mpango<br />
wa kuhujumu Uislamu ulioandaliwa katika ile semina ya Nairobi<br />
ya Septemba 23, 1989.<br />
Semina hiyo ambayo ilikuwa na mada moja kuu – “Kukabiliana<br />
na Uislamu” ilihudhuriwa na washiriki 989 toka mikoa yote ya Kenya<br />
isipokuwa mkoa wa Pwani (Mombasa).<br />
Msemaji Mkuu katika semina hiyo alikuwa Prof. Hafkean<br />
ambaye ni Profesa katika mambo ya Kiislamu Afrika na muanzilishi<br />
wa “Miradi ya Kiislamu Afrika” (Islam Projects in Africa).<br />
Profesa Hafkean alizungumza kwa kirefu imani na tabia za<br />
Waislamu na namna Wakristo wanavyoweza kuwavuruga Waislamu<br />
nchini Kenya. Katika jumla ya mikakati aliyoibainisha Profesa<br />
Hafkean iliyoandaliwa kupambana na Uislamu ni pamoja na:<br />
(i) Kwamba wadhamini wa chuo Kikuu cha Daystar Nairobi<br />
wametenga kiasi cha Paundi Milioni 56 sawa na kiasi cha<br />
shilingi 1.97 bilioni kuwasaidia vijana wa Kiislamu wanaoritadi.<br />
146