08.06.2013 Views

Download - islamic education panel

Download - islamic education panel

Download - islamic education panel

SHOW MORE
SHOW LESS

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

Pia ni wajibu kwa Waislamu kuingilia kati na kusuluhisha<br />

wawili waliogombana kama tunavyoamrishwa katika Qur-an:<br />

Na ikiwa makundi mawili katika Waislamu wanapigana,<br />

basi fanyeni suluhu baina yao, na ikiwa moja la hayo<br />

linamdhulumu mwenziwe, basi lipigeni lile linaloonea<br />

mpaka lirudi katika amri ya Mwenyezi Mungu. Na kama<br />

likirudi, basi yapatanisheni baina yao kwa uadilifu. Na<br />

hukumuni kwa haki.Hakika Mwenyezi huwapenda wanao<br />

hukumu kwa haki (49:9).<br />

(vi) Kushirikiana pamoja katika furaha na misiba<br />

Miongoni mwa wema unaojenga udugu na upendo miongoni<br />

mwa watu ni mtu kumpendelea mwenziwe lile analolipenda na<br />

kuchukia lisimfikie mwenziwe lile analolichukia. Aidha Waislamu<br />

wanalazimika kujumuika na Waislamu wenzao kwenye sherehe na<br />

furaha na kushiriki nao pia kwenye misiba na huzuni.<br />

(vii) Kuzuia vinavyodhuru visimfikie mwenzio<br />

Pamoja na Muislamu kuchukia baya lisimfike Muislamu<br />

mwenziwe, pia Muislamu atumie juhudi kadri ya uwezo wake<br />

kuzuia kwa hali na mali mabaya yasimfike Muislamu mwenziwe.<br />

Tunajifunza msisitizo wa jambo hili katika Hadith ifuatayo:<br />

Abu Barzata (r.a) ameeleza: “Nilisema: ‘Ee Mtume wa<br />

Allah! Nifundishe jambo ambalo litaninufaisha”. Alisema<br />

(Mtume): “Ondoa vitu vibaya (kama vile miba uchafu, n.k.)<br />

katika njia ya Waislamu”. (Muslim).<br />

91

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!