Download - islamic education panel
Download - islamic education panel
Download - islamic education panel
Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
(vii) Kusimama na kuonya ni amri ya kuwafahamisha<br />
watu juu ya upweke wa Allah (s.w) kuwa hapana Mola apasaye<br />
kuabudiwa kwa haki ila Allah na kisha kuwafahamisha namna ya<br />
kumuabudu Allah (s.w) pekee katika kila kipengele cha maisha.<br />
Baada ya kufikisha ujumbe huu wa Tawhiid, kwa hekima na<br />
mawaidha mazuri (rejea Qur-an 16:125), Mtume na Waumini kwa<br />
ujumla wanaamrishwa kuwaonya watu juu ya adhabu kali<br />
itakayowafika wale wote watakaoishi kinyume cha Tawhiid –<br />
katika maisha ya akhera.<br />
Pia amri hii ya kuwaonya watu inakwenda sambamba na<br />
kuwabashiria malipo mema watakayopata wasimamishaji wa<br />
Tawhiid katika maisha ya akhera. Kuufundisha Uislamu na kuweka<br />
wazi faida itakayopatikana kwa wale watakaoufuata vilivyo na<br />
hasara itakayowafika wale watakaoukanusha, ni hatua muhimu na<br />
ya msingi mno katika harakati za kusimamisha Uislamu katika<br />
jamii.<br />
(viii) Kutakasa nguo, ni amri inayoashiria kuwa mwenye<br />
kulingania Uislamu anatakiwa awe mfano wa kuigwa kwa tabia njema.<br />
Pamoja na mlinganiaji kutekeleza amri ya kutakasa nguo zake na<br />
mwili wake ili awe kivutio kwa watu atakaokutana nao katika harakati<br />
za kulingania Uislamu, anatakiwa awe na tabia njema itakayovuta<br />
usikivu wa watu. Katika kutekeleza amri hii Mtume (s.a.w) alikuwa<br />
akipendelea vazi jeupe na kujipaka manukato ili asiwe kero kwa watu<br />
kutokana na harufu mbaya inayotokana na nguo chafu na majasho.<br />
Sambamba na usafi huu wa nguo na mwili, Mtume (s.a.w)<br />
alikuwa na tabia njema kabisa.<br />
“Na bila shaka una tabia njema kabisa.” (68:4)<br />
56