08.06.2013 Views

Download - islamic education panel

Download - islamic education panel

Download - islamic education panel

SHOW MORE
SHOW LESS

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

(vii) Kusimama na kuonya ni amri ya kuwafahamisha<br />

watu juu ya upweke wa Allah (s.w) kuwa hapana Mola apasaye<br />

kuabudiwa kwa haki ila Allah na kisha kuwafahamisha namna ya<br />

kumuabudu Allah (s.w) pekee katika kila kipengele cha maisha.<br />

Baada ya kufikisha ujumbe huu wa Tawhiid, kwa hekima na<br />

mawaidha mazuri (rejea Qur-an 16:125), Mtume na Waumini kwa<br />

ujumla wanaamrishwa kuwaonya watu juu ya adhabu kali<br />

itakayowafika wale wote watakaoishi kinyume cha Tawhiid –<br />

katika maisha ya akhera.<br />

Pia amri hii ya kuwaonya watu inakwenda sambamba na<br />

kuwabashiria malipo mema watakayopata wasimamishaji wa<br />

Tawhiid katika maisha ya akhera. Kuufundisha Uislamu na kuweka<br />

wazi faida itakayopatikana kwa wale watakaoufuata vilivyo na<br />

hasara itakayowafika wale watakaoukanusha, ni hatua muhimu na<br />

ya msingi mno katika harakati za kusimamisha Uislamu katika<br />

jamii.<br />

(viii) Kutakasa nguo, ni amri inayoashiria kuwa mwenye<br />

kulingania Uislamu anatakiwa awe mfano wa kuigwa kwa tabia njema.<br />

Pamoja na mlinganiaji kutekeleza amri ya kutakasa nguo zake na<br />

mwili wake ili awe kivutio kwa watu atakaokutana nao katika harakati<br />

za kulingania Uislamu, anatakiwa awe na tabia njema itakayovuta<br />

usikivu wa watu. Katika kutekeleza amri hii Mtume (s.a.w) alikuwa<br />

akipendelea vazi jeupe na kujipaka manukato ili asiwe kero kwa watu<br />

kutokana na harufu mbaya inayotokana na nguo chafu na majasho.<br />

Sambamba na usafi huu wa nguo na mwili, Mtume (s.a.w)<br />

alikuwa na tabia njema kabisa.<br />

“Na bila shaka una tabia njema kabisa.” (68:4)<br />

56

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!