Download - islamic education panel
Download - islamic education panel
Download - islamic education panel
Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
Bani Khawaizin ambalo lina sifa ya usafi na lugha fasaha ya<br />
Kiarabu alitokea Taifu mji wenye hali nzuri ya hewa kwa kulelea<br />
watoto.Mtume alipata bahati ya kukaa miaka mine badala ya<br />
miwili kutokana na magonjwa ya milipuko yaliyojitokeza Makkah<br />
jambo ambalo lilimuwezesha kuzungumza kiarabu kwa ufasaha<br />
zaidi kuliko watu wengine wa Makkah. Mama yake Amina bint<br />
Wahhab alimlea mpaka alipofikisha umri wa miaka 6 akafariki.<br />
Babu yake Abdul-Muttalib aliendelea kumlea na alipofikisha umri<br />
wa miaka 8 akafariki. Kisha alilelewa na ‘Ami yake Abu Talib<br />
ambaye aliendelea kuwa naye mpaka alipopewa utume na alikuwa<br />
akimlinda mpaka alipofariki Mtume(s.a.w) akiwa na miaka kumi ya<br />
utume. Hii haikutokea tu kwa bahati nasibu, bali tunafahamishwa<br />
katika Qur-an kuwa ni maandalizi maalum aliyoyapanga Allah (s.w) .<br />
Je! Hakukukuta yatima akakupa makazi (mazuri ya kukaa)?<br />
(93:6).<br />
(iv) Tabia yake njema isiyo na mfano wake<br />
Tabia nzuri ya Mtume (s.a.w) haikuishia utotoni mwake tu<br />
iliendelea katika umri wake wote. Tunajifunza katika historia kuwa<br />
hata alipokuwa mtoto hakuwahi kufanya vitendo vya kipuuzi vya<br />
kitoto na alikuwa ni mwenye haya sana. Wakati fulani kuta za Ka’abah<br />
zilifanyiwa ukarabati. Wavulana wadogo wadogo nao wakashiriki<br />
katika kazi ya ukarabati. Wavulana hawa walizitoa nguo zao zakiunoni<br />
na kuziweka mabegani ili kubebea mawe. Abu Talib alimshauri Mtume<br />
(s.a.w) naye ajiunge na watoto wenziwe. Mtume (s.a.w) alikubaliana<br />
na ushauri wa Ami yake, lakini alikuwa na haya sana hata katika umri<br />
ule wa utotoni. Hivyo, alipojaribu naye kuvua nguo yake na kubaki<br />
uchi, alishikwa na bumbuazi (butwaa) na kuanguka chini.<br />
Mtume (s.a.w) tangu utotoni mwake aliepukana na tabia zote<br />
chafu zenye kuchukiza watu kwa ujumla. Pia aliepushwa na<br />
matendo yote maovu yenye kumchukiza Allah (s.w) ambayo<br />
43