08.06.2013 Views

Download - islamic education panel

Download - islamic education panel

Download - islamic education panel

SHOW MORE
SHOW LESS

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

Bani Khawaizin ambalo lina sifa ya usafi na lugha fasaha ya<br />

Kiarabu alitokea Taifu mji wenye hali nzuri ya hewa kwa kulelea<br />

watoto.Mtume alipata bahati ya kukaa miaka mine badala ya<br />

miwili kutokana na magonjwa ya milipuko yaliyojitokeza Makkah<br />

jambo ambalo lilimuwezesha kuzungumza kiarabu kwa ufasaha<br />

zaidi kuliko watu wengine wa Makkah. Mama yake Amina bint<br />

Wahhab alimlea mpaka alipofikisha umri wa miaka 6 akafariki.<br />

Babu yake Abdul-Muttalib aliendelea kumlea na alipofikisha umri<br />

wa miaka 8 akafariki. Kisha alilelewa na ‘Ami yake Abu Talib<br />

ambaye aliendelea kuwa naye mpaka alipopewa utume na alikuwa<br />

akimlinda mpaka alipofariki Mtume(s.a.w) akiwa na miaka kumi ya<br />

utume. Hii haikutokea tu kwa bahati nasibu, bali tunafahamishwa<br />

katika Qur-an kuwa ni maandalizi maalum aliyoyapanga Allah (s.w) .<br />

Je! Hakukukuta yatima akakupa makazi (mazuri ya kukaa)?<br />

(93:6).<br />

(iv) Tabia yake njema isiyo na mfano wake<br />

Tabia nzuri ya Mtume (s.a.w) haikuishia utotoni mwake tu<br />

iliendelea katika umri wake wote. Tunajifunza katika historia kuwa<br />

hata alipokuwa mtoto hakuwahi kufanya vitendo vya kipuuzi vya<br />

kitoto na alikuwa ni mwenye haya sana. Wakati fulani kuta za Ka’abah<br />

zilifanyiwa ukarabati. Wavulana wadogo wadogo nao wakashiriki<br />

katika kazi ya ukarabati. Wavulana hawa walizitoa nguo zao zakiunoni<br />

na kuziweka mabegani ili kubebea mawe. Abu Talib alimshauri Mtume<br />

(s.a.w) naye ajiunge na watoto wenziwe. Mtume (s.a.w) alikubaliana<br />

na ushauri wa Ami yake, lakini alikuwa na haya sana hata katika umri<br />

ule wa utotoni. Hivyo, alipojaribu naye kuvua nguo yake na kubaki<br />

uchi, alishikwa na bumbuazi (butwaa) na kuanguka chini.<br />

Mtume (s.a.w) tangu utotoni mwake aliepukana na tabia zote<br />

chafu zenye kuchukiza watu kwa ujumla. Pia aliepushwa na<br />

matendo yote maovu yenye kumchukiza Allah (s.w) ambayo<br />

43

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!