Download - islamic education panel
Download - islamic education panel
Download - islamic education panel
Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
kuiingiza katika utekelezaji wa maisha yake ya kila siku.<br />
Awe na ada ya kupitia Qur’an yote kwa namna hii<br />
kuanzia sura ya mwanzo (Al-Faati’ha)mpaka sura ya<br />
mwisho (An-Naas)na kuanza tena mzunguko huo dumu<br />
daima. Katika kupitia Qur’an kwa namna hii,<br />
mwanaharakati awe na daftari maalumu la kunukuu<br />
mafunzo maalumu atakayo yapata. Ni kawaida, kila<br />
utakapoipitia Qur’an, hutaacha kupata mafunzo mapya<br />
kulingana na mazingira na wakati uliopo.<br />
(vi) Kuwa na ada ya kumdhukuru (kumkumbuka) na<br />
kumtukuza Allah (s.w) mara kwa mara kwa kuleta<br />
dhikiri asubuhi na jioni na katika kufanya matendo<br />
maalumu kama vile kulala na kuamka, kuanza na<br />
kumaliza kula na kadhalika, kama alivyofanya Mtume<br />
(s.a.w). Rejea Darasa la Watu Wazima Juzuu ya tatu –<br />
sura ya tano.<br />
(vii)Kumtegemea Allah (s.w) na kumfanya mlinzi pekee.<br />
Mwanaharakati hatamchalea au kumuogopa yeyote<br />
anayemsalitisha na Allah (s.w) na Mtume wake.<br />
(viii)Kuwa na tabia ya kujihesabu na kuleta toba ya kweli<br />
pale anapogundua amemkosea Allah (s.w) na Mtume<br />
wake. Kuwa na kawaida ya kuleta stighfar mara 100 au<br />
zaidikila siku.<br />
5. Kujihusisha na masuala ya kijamii kwa kufanya<br />
yafuatayo:<br />
(i) Kuwa mwepesi wa kuwatendea wema na kutoa huduma<br />
kwa wanaadamu wenzake kila inapohitajika.<br />
(ii)Kuwa mstari wa mbele katika kazi za kujitolea za<br />
kuendeleza Uislamu na jamii ya binaadamu kwa ujumla<br />
kwa kutarajia malipo kutoka kwa Allah (s.w) tu.<br />
(iii)Kuwa mwepesi wa kutoa mali kwa ajili ya kuendeleza<br />
harakati za Kiislamu na kuwasaidia wenye matatizo<br />
(wenye kuhitajia msaada) kwa kutarajia malipo kutoka<br />
kwa Allah (s.w) tu.<br />
79