08.06.2013 Views

Download - islamic education panel

Download - islamic education panel

Download - islamic education panel

SHOW MORE
SHOW LESS

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

katika jamii. Kila shughuli anayoifanya katika harakati za maisha yake<br />

ya kila siku iwe na lengo la kumuwezesha kusimamisha Uislamu na<br />

kuufanya uwe juu ya mifumo mingine yote ya maisha. Hili ndilo lengo<br />

kuu la kuletwa Mtume (s.a.w) kama inavyobainishwa katika Qur’an:<br />

Yeye ndiye aliyemleta Mtume wake kwa uongofu na Dini ya<br />

haki, ili aijaalie kushinda dini zote ijapokuwa watachukia<br />

washirikina (9:33,61 :9)<br />

5. Kutarajia malipo kutoka kwa Allah (s. w) tu.<br />

Mwanaharakati wa Kiislamu hana budi kulifahamu vema<br />

lengo hili kuu la kusimamisha Uislamu katika jamii na awe na<br />

yakini kuwa kwa kuliendea lengo hili anafanya biashara na Allah<br />

(s.w) kama inavyobainishwa katika Qur’an:<br />

Mwenyezi Mungu amenunua kwa waumini nafsi zao na mali<br />

zao ili naye awape pepo. Na wanapigana katika njia ya<br />

Allah. Wanaua na wanauawa. Hii ndiyo ahadi<br />

aliyojilazimisha (Mwenyezi Mungu) katika Taurati,Injili na<br />

Quran.Na ni nani atekelezaye zaidi ahadi kuliko Mwenyezi<br />

Mungu? Basi furahini kwa biashara mliyofanya naye. Na<br />

huko ndiko kufuzu kuliko kukubwa.(9: 111)<br />

70

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!