08.06.2013 Views

Download - islamic education panel

Download - islamic education panel

Download - islamic education panel

SHOW MORE
SHOW LESS

You also want an ePaper? Increase the reach of your titles

YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.

Kutokana na aya hizi, Uislamu ni mwepesi kuujua kwa<br />

anayetaka kuujua na pia ni mwepesi kuutekeleza kwa kuwa ni dini<br />

nayolandana na maumbile binaadamu:<br />

“Basi uelekeze uso wako katika Dini iliyo sawasawa – ndilo<br />

umbile Mwenyezi Mungu alilowaumbia watu: (yaani Dini hii ya<br />

Kiislamu inawafikiana barabara na umbo la binaadamu). Hakuna<br />

mabadiliko katika maumbile ya viumbe vya Mwenyezi Mungu.<br />

Hiyo ndiyo Dini iliyo haki, lakini watu wengi hawajui” (30:30).<br />

Yapo mambo kadhaa yakizingatiwa yatamuwezesha<br />

Muislamu kuujua Uislamu kwa usahihi na kuutekeleza kwa wepesi.<br />

Baadhi ya mazingatio hayo ni haya yafuatayo:<br />

(i) Kujiwekea ratiba ya kujisomea Maarifa ya Uislamu.<br />

(ii) Kusoma kwa lengo kwa kufuata Mtaala.<br />

(iii) Kusoma kwa njia ya mjadala (Darasa Duara).<br />

(iv) Kujiunga na Elimu ya Kiislamu kwa Posta(E.K.P)<br />

(v) Kusoma Qur’an kwa mazingatio.<br />

Kuweka ratiba ya kujisomea.<br />

Watu kwa kujua thamani ya elimu ya mazingira hujipinda<br />

katika kuitafuta, hutoa gharama kubwa na kutumia muda mwingi.<br />

Elimu ya Mwongozo ambayo ndiyo dira ya maisha ya<br />

binaadamu ya hapa duniani na akhera inapaswa iwe na thamani<br />

kubwa zaidi kwani elimu ya mazingira bila ya kufuata mwongozo<br />

wa Allah (s.w) huangamiza badala ya kunufaisha.<br />

Pamoja na ukweli huu Waislamu waliowengi hufanya<br />

jitihada ndogo sana katika kujifunza Uislamu na mara nyingi<br />

hawapati nafasi kabisa. Kwa kujua thamani ya kusoma elimu ya<br />

mwongozo kwa ajili ya Allah (s.w) hatunabudi kusoma kwa<br />

201

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!