08.06.2013 Views

Download - islamic education panel

Download - islamic education panel

Download - islamic education panel

SHOW MORE
SHOW LESS

You also want an ePaper? Increase the reach of your titles

YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.

Na lau kama tungalifanya Qur’an kwa lugha isiyo ya<br />

Kiarabu wangalisema: “Kwa nini Aya zake<br />

hazikupambanuliwa? Lo! Lugha isiyokuwa ya Kiarabu na<br />

(Mtume) Muarabu! (Mambo gani haya)!” Sema: “Hii<br />

(Qur’an) ni uwongofu na poza kwa wale walioamini; na<br />

wale wasioamini umo uzito katika masikio yao; na hiyo<br />

(Qur’an) ni giza kwao. (Hawasikii. Kama kwamba) hao<br />

wanaitwa, na hali ya kuwa wako mbali kabisa. “ (41:44)<br />

Kwa mnasaba wa ujumbe wa aya hii, nasi watu<br />

watatushangaa kuwafikishia ujumbe wa Uislamu kwa lugha<br />

wasiyoifahamu. Mtume (s.a.w) mwenyewe aliwahimiza<br />

maswahaba zake alipowatuma kutoa Da’awah kwa watu mbali<br />

mbali wasiokuwa waarabu kuwa wajifunze lugha zao na<br />

wawafikishie ujumbe wa Uislamu kwa lugha zao. Hivyo watu<br />

kutokuwa waarabu au kutojua kiarabu isiwe sababu ya kuwafanya<br />

wasifikiwe na ujumbe sahihi wa Uislamu.<br />

6. Kujadiliana na watu kwa namna iliyo bora<br />

Mlinganiaji anatakiwa atumie lugha ya upendo na mvuto<br />

itakayoweza kuvuta nyoyo na usikivu wa watu anaowalingania.<br />

Asiwalazimishie watu ujumbe bali awavutie kwa kutoa hoja zenye<br />

mashiko madhubuti kama Allah (s.w) anavyo tuelekeza:<br />

“Hakuna kulazimishwa (mtu kuingia) katika dini. Uongofu<br />

umekwisha pambanuka na upotofu. Basi anayemkataa<br />

twaaghuut na akamwamini Mwenyezi Mungu, bila shaka yeye<br />

ameshika kishiko chenye nguvu kisichovunjika. Na Mwenyezi<br />

Mungu ni Mwenye kusikia, Mwenye kujua. “(2:256)<br />

131

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!