08.06.2013 Views

Download - islamic education panel

Download - islamic education panel

Download - islamic education panel

SHOW MORE
SHOW LESS

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

9. Kuwa na Hekima<br />

Kama ilivyo kwa mwanaharakati binafsi, kundi la Harakati<br />

linalazimika kuendesha Harakati kwa hekima, kwa kufanya<br />

mambo ya sawasawa yanayolandana na Qur’an na Sunnah, kwa<br />

namna ya sawa sawa kwa wakati wa sawa sawa katika mazingira<br />

muafaka.<br />

Vile vile ni katika hekima kwa kundi la Harakati kuyafahamu<br />

vyema matatizo yanayoikabili jamii ya Waislamu hata isiweze<br />

kusimamisha Uislamu, kuchukua njia sahihi ya kuyatatua, kwa<br />

kuzingatia wakati na mazingira.<br />

Kundi la Harakati litakapojitahidi kwa kadiri<br />

itakavyowezekana kusifika kwa sifa hizi tisa(9),hapanashaka kwa<br />

taufiiq ya Allah(s.w),litakuwa lile kundi aliloagiza Allah(s.w)<br />

(Qur’an 3:104) lililoweza kulingania kheri, kuamrisha mema na<br />

kukataza mabaya katika jamii.<br />

Kuanzisha kundi la harakati kama alivyofanya<br />

Mtume(s.a.w)<br />

Tukirejea historia tunaona kuwa Mtume (s.a.w) kabla ya<br />

Utume aliandaliwa Ki-il-hamu tangu utotoni na alipambika na<br />

tabia njema isiyo na mfano wake katika jamii yake. Alipopewa amri<br />

ya kulingania Uislamu alianza na familia yake, kisha kwa marafiki<br />

na jamaa zake wa karibu. Wale walioukubali Uislamu katika jamaa<br />

na rafiki zake hao nao waliulingania Uislamu kwa familia zao,<br />

rafiki na jamaa zao wa karibu. Mtume (s.a.w) alianzisha darasa<br />

duara la kuwafunza Uislamu kinadharia na kimatendo wale wote<br />

waliosilimu katika nyumba ya Bwana Arkam bin Abi-Arqam.<br />

Darasa hili la Mtume (s.a.w) lilizaa kundi madhubuti lililokuwa<br />

chachu ya kusimamisha Dola ya Kiislamu iliyofanya Dini ya Allah<br />

(s.w) kuwa juu ya mifumo yote ya maisha katika kipindi cha miaka<br />

23 tu. Hivyo kwa kufuata Minhaji hii ya Mtume (s.a.w), tutaanzisha<br />

kundi la Harakati lililo madhubuti kwa kufuata Hatua zifuatazo:<br />

108

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!