Download - islamic education panel
Download - islamic education panel
Download - islamic education panel
Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
9. Kuwa na Hekima<br />
Kama ilivyo kwa mwanaharakati binafsi, kundi la Harakati<br />
linalazimika kuendesha Harakati kwa hekima, kwa kufanya<br />
mambo ya sawasawa yanayolandana na Qur’an na Sunnah, kwa<br />
namna ya sawa sawa kwa wakati wa sawa sawa katika mazingira<br />
muafaka.<br />
Vile vile ni katika hekima kwa kundi la Harakati kuyafahamu<br />
vyema matatizo yanayoikabili jamii ya Waislamu hata isiweze<br />
kusimamisha Uislamu, kuchukua njia sahihi ya kuyatatua, kwa<br />
kuzingatia wakati na mazingira.<br />
Kundi la Harakati litakapojitahidi kwa kadiri<br />
itakavyowezekana kusifika kwa sifa hizi tisa(9),hapanashaka kwa<br />
taufiiq ya Allah(s.w),litakuwa lile kundi aliloagiza Allah(s.w)<br />
(Qur’an 3:104) lililoweza kulingania kheri, kuamrisha mema na<br />
kukataza mabaya katika jamii.<br />
Kuanzisha kundi la harakati kama alivyofanya<br />
Mtume(s.a.w)<br />
Tukirejea historia tunaona kuwa Mtume (s.a.w) kabla ya<br />
Utume aliandaliwa Ki-il-hamu tangu utotoni na alipambika na<br />
tabia njema isiyo na mfano wake katika jamii yake. Alipopewa amri<br />
ya kulingania Uislamu alianza na familia yake, kisha kwa marafiki<br />
na jamaa zake wa karibu. Wale walioukubali Uislamu katika jamaa<br />
na rafiki zake hao nao waliulingania Uislamu kwa familia zao,<br />
rafiki na jamaa zao wa karibu. Mtume (s.a.w) alianzisha darasa<br />
duara la kuwafunza Uislamu kinadharia na kimatendo wale wote<br />
waliosilimu katika nyumba ya Bwana Arkam bin Abi-Arqam.<br />
Darasa hili la Mtume (s.a.w) lilizaa kundi madhubuti lililokuwa<br />
chachu ya kusimamisha Dola ya Kiislamu iliyofanya Dini ya Allah<br />
(s.w) kuwa juu ya mifumo yote ya maisha katika kipindi cha miaka<br />
23 tu. Hivyo kwa kufuata Minhaji hii ya Mtume (s.a.w), tutaanzisha<br />
kundi la Harakati lililo madhubuti kwa kufuata Hatua zifuatazo:<br />
108