08.06.2013 Views

Download - islamic education panel

Download - islamic education panel

Download - islamic education panel

SHOW MORE
SHOW LESS

You also want an ePaper? Increase the reach of your titles

YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.

mipango yenye kupelekea kufikia lengo kuu la kusimamisha<br />

Uislamu katika jamii.<br />

(xi) Utegemezi kwa Allah (s.w)<br />

Kiongozi na wale anaowaongoza wawe na tabia ya<br />

kumtanguliza Allah (s.w) kwa kila walifanyalo kwa kumtegemea<br />

yeye na kuchunga maamrisho na makatazo yake.<br />

(xii) Msimamo katika Kuendea Lengo<br />

Kiongozi wa Kiislamu anatakiwa awe na msimamo thabiti<br />

katika kuendea lengo na wala asisukumwe na maslahi binafsi iwe<br />

ya vitu au sifa. Kiongozi asiyeyumbishwa na maslahi binafsi<br />

hujijengea mazingira ya kuaminika hivyo kupata watu wengi zaidi<br />

kwa kushiriki katika kazi ya Da’awah.<br />

(xiii) Mwenye kuzingatia maelekezo ya Shura<br />

Ni muhimu kwa kiongozi wa Kiislamu kuzingatia maelekezo<br />

ya shura katika uongozi wake. Asimamie utekelezaji wa maamuzi<br />

ya shura na pale maamuzi hayo yatakapokuwa hayatekelezeki,<br />

ayarudishe kwenye shura.<br />

(xiv) Mwenye Kujiamini<br />

Kiongozi wa Kiislamu anatakiwa awe na uwezo wa kujenga<br />

mazingira ambayo yatamruhusu kila mtu kutoa mawazo yake kwa<br />

uhuru. Hili haliwezi kupatikana iwapo kiongozi hajiamini.<br />

Kiongozi atajiamini iwapo atadumu katika Ucha-Mungu na<br />

uadilifu.<br />

(xv) Uwezo wa Kuainisha Matatizo na Kuyatafutia<br />

Ufumbuzi<br />

Kiongozi ni lazima awe na uwezo wa kutambua matatizo<br />

yanayoikabili jamii yake. Hili ni muhimu kwa sababu kulitambua<br />

tatizo ni hatua muhimu sana katika kuendea utatuzi wake. Hatua<br />

hii huanza kwa kulifafanua tatizo. Katika kuainisha tatizo ni<br />

197

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!