08.06.2013 Views

Download - islamic education panel

Download - islamic education panel

Download - islamic education panel

SHOW MORE
SHOW LESS

You also want an ePaper? Increase the reach of your titles

YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.

Naye ndiye aliyekujaalieni kuwa Makhalifa (viongozi) katika<br />

ardhi. Na amewanyanyua baadhi yenu juu ya wengine daraja<br />

kubwa kubwa ili akufanyieni mtihani kwa hayo aliyokupeni.<br />

Hakika Mola wako ni mwepesi wa kuhisabu na hakika yeye ni<br />

mwingi wa kusamehe, mwingi wa kurehemu. (6:165)<br />

Kutokana na aya hii tunajifunza kuwa kiongozi anatakiwa<br />

mara zote afahamu kuwa wadhifa wa uongozi alionao ni mtihani<br />

kwake. Allah (s.w) amemuinua daraja na kumfanya kiongozi juu<br />

ya wengine ili kumfanyia mtihani kuwa atashukuru neema hiyo<br />

aliyotunukiwa na Mola wake kwa kutekeleza wajibu wake ipasavyo<br />

na kuchunga mipaka ya Allah (s.w) katika kazi hiyo au atakufuru<br />

ajipe uungu kwa kuchupa mipaka ya Allah na kuwageuza watumwa<br />

wake wale waliomchagua na kumfanya kiongozi wao. Kiongozi<br />

anatakiwa awe msaada na rehema kwa wale anaowaongoza na wala<br />

asiwe mzigo na tatizo kwa raia zake hao. Mtume (s.a.w) kila<br />

alipowachagua sahaba zake kuwa viongozi wa sehemu mbali mbali<br />

daima alikuwa akiwausia kuwa watu wa msaada na wenye huruma<br />

na upole kwa ria zao.<br />

(vi) Uadilifu<br />

Kiongozi wa Kiislamu anatakiwa awe muadilifu. Kipimo cha<br />

kiongozi mzuri ni uadilifu. Kiongozi wa Kiislamu akiwa muadilifu<br />

huwa Khalifa wa Allah (s.w) na akiwa si muadilifu huwa Khalifa wa<br />

Shetani. Uadilifu unasisitizwa mno katika Qur-an kama<br />

tunavyojifunza katika aya zifuatazo:<br />

..........<br />

Kwa hakika Mwenyezi Mungu anaamrisha uadilifu…...... (16:90)<br />

193

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!