08.06.2013 Views

Download - islamic education panel

Download - islamic education panel

Download - islamic education panel

SHOW MORE
SHOW LESS

You also want an ePaper? Increase the reach of your titles

YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.

yalionekana mazuri mbele za watu wa jamii yake. Kwa mfano<br />

katika umri wa ujana wake aliazimia mara mbili kuhudhuria<br />

mikesho ya ngoma za harusi za rafiki zake wawili lakini Allah (s.w)<br />

alimwepusha na mikesha hiyo kwa kumpa usingizi mzito mpaka<br />

asubuhi kwa safari zote mbili.<br />

Tangu utotoni mwake Mtume (s.a.w) alichukia sana Ibada ya<br />

masanamu. Hakupata kuhudhuria hata mara moja ibada za<br />

masanamu wala hakupata kula kilichoandaliwa kwa ajili ya<br />

masanamu. Moyo wake pia ulichukia maovu yote mengine<br />

yaliyofanywa matendo ya kawaida na watu wa jamii yake kama vile<br />

ulevi, uzinifu, uchezaji kamari, ulaji riba, udhalimu, ulaji wa<br />

vyakula vya haramu, n.k.<br />

Tangu utotoni mwake, Muhammad (s.a.w) alisifika kwa kila<br />

sifa nzuri zilizobainishwa katika Qur’an. Bibi ‘Aisha (r.a)<br />

alipoulizwa juu ya tabia ya Mtume (s.a.w) alijibu kuwa tabia yake<br />

ni Qur’an. Yaani Mtume (s.a.w) amejipamba na vipengele vyote vya<br />

tabia njema vilivyobainsihwa katika Qur’an tangia utotoni mwake.<br />

Qur’an yenyewe katika miongoni mwa aya zake za mwanzo<br />

mwanzo kushuka, inamsifu Mtume (s.a.w) kwa tabia yake tukufu:<br />

“Na bila shaka unatabia njema kabisa” (68:4)<br />

Aya hii haielezi kuwa tabia yake ilikuwa njema tu pale<br />

alipopata utume bali inaashiria kuwa tabia yake njema anayo tangu<br />

utotoni mwake. Muhammad (s.a.w) tangu utotoni mwake tumeona<br />

kuwa alikuwa mpole, mtulivu, mwenye huruma, mwenye haya na<br />

mwenye sifa zote nzuri zilizowapendeza watu na kuwavutia.<br />

Alikuwa mashuhuri Bara Arab nzima kwa ukweli na uaminifu<br />

wake. Alikuwa mkweli mno mpaka akapewa jina la “As-Sadiq” –<br />

“mkweli” na alikuwa mwaminifu mno mpaka akapewa jina la Al-<br />

Amin. Muhammad (s.a.w) alikuwa haitwi ila kwa jina la As-Sadiq<br />

44

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!