Download - islamic education panel
Download - islamic education panel
Download - islamic education panel
Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
kisimamo cha usiku (Qiyamullayl) ni ili tupate maandalizi ya<br />
“Ukomandoo” (Ujasiri wa nafsi) yatakayotuwezesha kukabiliana<br />
na suluba (misuko suko) ya kusimamisha Uislamu katika jamii.<br />
Allah (s.w) anabainisha pia kuwa maandalizi haya hayafai mchana<br />
ila usiku kwa sababu kuna mazingira mazuri ya utulivu<br />
yatakayompelekea huyu askari wa Allah kuwa na khushui<br />
(unyenyekevu) ya hali ya juu inayohitajika kuomba hidaya na<br />
msaada kutoka kwa Allah (s.w). Pia kuamka usiku na kukatisha<br />
utamu wa usingizi katika theluthi ya mwisho ya usiku, humpa<br />
Muislamu zoezi la uvumilivu na subira. Hivyo, ni wazi kuwa,<br />
kisimamo cha usiku, kikitekelezwa vilivyo, kinauwezo mkubwa<br />
wa kumfanya Muislamu awe na ujasiri wa kusimamisha Uislamu<br />
katika jamii kwa hali yoyote iwayo. Hivyo kwa waumini wa kweli,<br />
wanaojua kuwa wanadhima ya kuusimamisha Uislamu katika<br />
jamii na kuuhami usiporomoke baada ya kusimama, kisimamo<br />
cha usiku, si jambo la khiari kwao kama Mola wao<br />
anavyowatanabahisha:<br />
Je, afanyae Ibada nyakati za usiku kwa kusujudu na<br />
kusimama na kuogopa Akhera na kutarajia rehema<br />
ya Mola wake (ni sawa na asiyefanya hayo)? Sema:<br />
“Je, wanaweza kuwa sawa wale wanaojua na wale<br />
wasiojua?” Wanaoatanabahi ni wale wenye akili<br />
tu. “(39:9)<br />
(iii) Kusoma Qur-an kwa mazingatio, kwa lengo la<br />
kuifanya kuwa dira pekee ya maisha yetu ya kila siku, ni nyenzo<br />
nyingine itakayotuwezesha kusimamisha Uislamu katika jamii.<br />
Uislamu ni mfumo wa maisha wa kutii na kufuata utaratibu wa<br />
kuendesha maisha ya kibinafsi na ya kijamii anaouridhia Allah<br />
(s.w).<br />
54