08.06.2013 Views

Download - islamic education panel

Download - islamic education panel

Download - islamic education panel

SHOW MORE
SHOW LESS

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

wema na wacha-Mungu, daima atajiona kuwa hajafanya wema<br />

wowote wa kumfanya ahisi kuwa bora kuliko wengine.<br />

Tumehimizwa katika Qur-an (83:26) tushindane katika mema na<br />

tuharakie mambo mema. Wala tusitosheke kwa mema machache<br />

tunayoyafanya.<br />

7. Kujiepusha na Ria<br />

Ria ni ugonjwa mwingine unaoweza kumtoa mtu katika<br />

Uislamu na kumtumbukiza katika ushirikina na unafiki.<br />

Muislamu anatakiwa afanye kila kitendo chema kwa ajili ya Allah<br />

(s.w) kwa matarajio ya kupata malipo kutoka Kwake tu na wala<br />

asifanye wema ili kujionyesha kwa watu. Mtu anayefanya wema<br />

kuwaonyesha watu, hayuko tayari kufanya wema pale ambapo<br />

hapana watu wa kumuona au kumsifu. Muislamu anatakiwa<br />

akumbuke daima kuwa yuko pamoja na Allah (s.w) kila wakati,<br />

naye ndiye mlipaji kwa kila analolifanya na anayajua hata yale ya<br />

siri yaliyoko katika nafsi yake.<br />

Kundi la Harakati halina budi kujiepusha na kujiweka mbali<br />

na ria. Halina budi kufanya mambo yake kwa siri kila<br />

iwezekanavyo. Ikibidi Mwanaharakati au kundi la Harakati lifanye<br />

shughuli zake hadharani, halina budi kujizuia na hisia za kujioa na<br />

kujitukuza kwa kutangaza mazuri yake linaloifanyia jamii.<br />

Katika juhudi za kujiepusha na ria, kila Mwanaharakati<br />

ajitahidi kuficha amali zake njema ambazo hazina lazima ya<br />

kuonekana. Kila mara Mwanaharakati atathmini hisia zake kuwa<br />

anafurahia na kupanda kichwa anaposifiwa na watu wakati<br />

inapobidi afanye wema hadharani, au anafurahia zaidi akifanya<br />

amali zake bila ya kuonekana na watu? Iwapo Mwanaharakati<br />

atagundua kuwa nafsi yake inapendelea kusifiwa na watu, basi<br />

ajirudi haraka na kutubia kwa Mola wake. Hali kadhalika, iwapo<br />

Mwanaharakati atakuwa hafanyi vizuri shughuli zake njema<br />

anapokuwa faraghani kama anavyozifanya akiwa hadharani,<br />

ajirudi haraka na kujihesabu kuwa amefanya ria na atubu haraka<br />

kwa Mola wake.<br />

106

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!