Download - islamic education panel
Download - islamic education panel
Download - islamic education panel
Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
wema na wacha-Mungu, daima atajiona kuwa hajafanya wema<br />
wowote wa kumfanya ahisi kuwa bora kuliko wengine.<br />
Tumehimizwa katika Qur-an (83:26) tushindane katika mema na<br />
tuharakie mambo mema. Wala tusitosheke kwa mema machache<br />
tunayoyafanya.<br />
7. Kujiepusha na Ria<br />
Ria ni ugonjwa mwingine unaoweza kumtoa mtu katika<br />
Uislamu na kumtumbukiza katika ushirikina na unafiki.<br />
Muislamu anatakiwa afanye kila kitendo chema kwa ajili ya Allah<br />
(s.w) kwa matarajio ya kupata malipo kutoka Kwake tu na wala<br />
asifanye wema ili kujionyesha kwa watu. Mtu anayefanya wema<br />
kuwaonyesha watu, hayuko tayari kufanya wema pale ambapo<br />
hapana watu wa kumuona au kumsifu. Muislamu anatakiwa<br />
akumbuke daima kuwa yuko pamoja na Allah (s.w) kila wakati,<br />
naye ndiye mlipaji kwa kila analolifanya na anayajua hata yale ya<br />
siri yaliyoko katika nafsi yake.<br />
Kundi la Harakati halina budi kujiepusha na kujiweka mbali<br />
na ria. Halina budi kufanya mambo yake kwa siri kila<br />
iwezekanavyo. Ikibidi Mwanaharakati au kundi la Harakati lifanye<br />
shughuli zake hadharani, halina budi kujizuia na hisia za kujioa na<br />
kujitukuza kwa kutangaza mazuri yake linaloifanyia jamii.<br />
Katika juhudi za kujiepusha na ria, kila Mwanaharakati<br />
ajitahidi kuficha amali zake njema ambazo hazina lazima ya<br />
kuonekana. Kila mara Mwanaharakati atathmini hisia zake kuwa<br />
anafurahia na kupanda kichwa anaposifiwa na watu wakati<br />
inapobidi afanye wema hadharani, au anafurahia zaidi akifanya<br />
amali zake bila ya kuonekana na watu? Iwapo Mwanaharakati<br />
atagundua kuwa nafsi yake inapendelea kusifiwa na watu, basi<br />
ajirudi haraka na kutubia kwa Mola wake. Hali kadhalika, iwapo<br />
Mwanaharakati atakuwa hafanyi vizuri shughuli zake njema<br />
anapokuwa faraghani kama anavyozifanya akiwa hadharani,<br />
ajirudi haraka na kujihesabu kuwa amefanya ria na atubu haraka<br />
kwa Mola wake.<br />
106