08.06.2013 Views

Download - islamic education panel

Download - islamic education panel

Download - islamic education panel

SHOW MORE
SHOW LESS

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

(d) Baada ya kupata kwa uwazi ujumbe wa Qur’an hatuna<br />

budi kuyaingiza maagizo ya Mola wetu katika utendaji<br />

huku tukimfanya Mtume (s.a.w) kiigizo chetu.<br />

(e) Kuisoma Qur’an mara kwa mara kuanzia mwanzo<br />

(Suratul Fatha) hadi mwisho (Suratul An-Naas) na<br />

msomaji awe na kalamu na daftari ya kuandika kila<br />

analoona ni muhimu au geni linalotaka kudhibitiwa –<br />

Hata Mtume (s.a.w) alisomewa Qur’an (4:41),<br />

akaiona kama ngeni kwake.<br />

(f) Tunaposoma Qur’an, tudhibiti kila tunachokipitia. Kama<br />

vile sifa zote ambazo kila mtu anataka asifike nazo. Na vile<br />

vile kuzidhibiti sifa zote ambazo anatakiwa mtu ajiepushe<br />

nazo. Tunaposoma Qur’an tudhibiti mambo ambayo<br />

Qur’an inasema kuwa kwa mambo hayo ndio<br />

kunapatikana mafanikio, na kwamambo hayo mengine<br />

ndio kunapatikana kuharibikiwa (maangamizo).<br />

(h) Tuwe na tabia ya kuirejea Qur’an kila tunapokabiliwa na<br />

tatizo lolote la kibinafsi au la kijamii.<br />

Tusiridhike kujifanyia au kufuata mkumbo katika kuendea<br />

mambo yetu ya kibinafsi au ya kijamii bila ya kuangalia<br />

kwanza Allah (s.w) kasema nini au kaagiza nini juu ya jambo<br />

hilo au Mtume wake (s.a.w) ambaye ndiye Mfasiri Mkuu wa<br />

Qur’an, ameliendeaje jambo hilo huku tukizingatia usia wa<br />

Mtume (s.a.w) alioutoa mwezi 9 Dhul-Haj, 10A.H katika<br />

uwanja wa Arafa pale alipokuwa anawaaga Waislamu na<br />

kusema:<br />

“Nimekuachieni vitu viwili ambavyo mkishikamana navyo<br />

hamtapotea abadan; navyo ni Kitabu cha Allah (Al-Qur’an)<br />

na Sunnah ya Mtume Wake”.<br />

207

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!