Download - islamic education panel
Download - islamic education panel
Download - islamic education panel
Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
Mwenyezi Mungu amenunua kwa Waumini nafsi zao na<br />
mali zao (watoe nafsi zao na mali zao katika kupigania<br />
Dini) ili na yeye awape Pepo. Wanapigana katika njia ya<br />
Mwenyezi Mungu; wanaua na wanauawa. Hii ndiyo<br />
ahadi aliyojilazimisha (Mwenyezi Mungu) katika Taurati<br />
na Injili na Qur-an. Na ni nani atekelezaye zaidi ahadi<br />
yake kuliko Mwenyezi Mungu? Basi furahini kwa<br />
biashara yenu mliyofanya naye (Mwenyezi Mungu). Na<br />
huko ndiko kufuzu kukubwa. “(9:111)<br />
Enyi mlioamini! Je! Nikujulisheni biashara<br />
itakayokuokoeni na adhabu iumizayo?<br />
(Biashara yenyewe ni hii) Muaminini Mwenyezi<br />
Mungu na Mtume wake, na piganieni Dini ya<br />
Mwenyezi Mungu kwa mali zenu na nafsi zenu.<br />
Haya ni bora kwenu ikiwa mnajuwa (61:10-11)<br />
(xi) Kufanya Subira kwa ajili ya Allah, ni nyenzo<br />
nyingine ya msingi itakayowawezesha Waumini kusimamisha<br />
Uislamu katika jamii. Katika harakati za kusimamisha Uislamu katika<br />
jamii, kuna kero na bughudha nyingi zinazoandaliwa na kusimamiwa<br />
na wapinzani wa Uislamu. Ukirejea historia ya Mtume (s.a.w), kero<br />
hizi huanza na kujenga mazingira ya kukatisha tamaa. Katika<br />
mazingira hayo, Mtume (s.a.w) aliitwa mwongo, mwenda wazimu,<br />
mtunga mashairi, mchawi, aliyepagawa, mkatikiwa na kheri (Abtari),<br />
n.k.<br />
Katika mazingira ya sasa makafiri wanajitahidi kuwa katisha<br />
tamaa wanaharakati kwa kuwaita siasa kali (fundamentalist),<br />
58