08.06.2013 Views

Download - islamic education panel

Download - islamic education panel

Download - islamic education panel

SHOW MORE
SHOW LESS

You also want an ePaper? Increase the reach of your titles

YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.

Kutokana na aya hizi tunajifunza kuwa Amri ya kwanza<br />

aliyopewa Mtume (s.a.w), na kwa hiyo waumini wote wa Ummah<br />

wake, ni kusoma au kutafuta elimu kwa ajili ya Allah (s.w). Kusoma<br />

kwa jina la Allah ni kusoma kwa lengo la kumuwezesha muumini<br />

kumjua na kumuabudu Mola wake vilivyo kisha kusimamisha<br />

Ukhalifa katika jamii.<br />

Katika mazingira ya kupewa amri hii ya kwanza, pale<br />

pangoni Hira katika kilima cha Nuur (Jabal-Nuur), Mtume (s.a.w)<br />

alishinikizwa kusoma na Malaika Jibril kwa kumbana<br />

(kumkumbatia kwa nguvu) mara tatu pale alipojitetea kuwa hajui<br />

kusoma. Kubanwa huku kwa Mtume (s.a.w) na Malaika Jibril<br />

kunaashiria kuwa elimu kwa waumini ni amri ya kwanza<br />

inayotakiwa kutekelezwa kwa hima na kwa taklifu kubwa.<br />

Hivyo Elimu ni amri ya kwanza inayotakiwa itekelezwe kwa<br />

juhudi na bidii zote. Ndiyo silaha kuu itakayowawezesha waumini<br />

kupata ushindi wa kusimamisha Uislamu katika jamii. Tukirejea<br />

nyuma katika historia, takrima ya kwanza aliyofanyiwa Adam (a.s)<br />

na Mola wake, ili kuandaliwa kuwa khalifa wa Allah (s.w) hapa<br />

duniani ni kufundishwa majina ya vitu vyote. Bimaana fani zote za<br />

Elimu anazohitajia binaadamu ili aweze kuwa kiongozi wa dunia<br />

kwa niaba ya Allah (s.w). Pia tunajifunza kuwa chanzo cha fani<br />

zote za elimu ni Allah (s.w).<br />

(ii) Suratul-Muzzammil (73:1-10)<br />

“Ewe uliyejifunika maguo simama usiku kucha<br />

(kuswali) ila muda mdogo (tu hivi). Nusu yake au<br />

upunguze kidogo au uzidishe na soma Qur-an<br />

vilivyo. (73:1-4)<br />

50

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!