08.06.2013 Views

Download - islamic education panel

Download - islamic education panel

Download - islamic education panel

SHOW MORE
SHOW LESS

You also want an ePaper? Increase the reach of your titles

YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.

Nu’maan bin Bashir (r.a.) ameeleza kuwa Mtume wa Allah<br />

amesema: “Mfano wa yule asiyekemea maovu na yule<br />

anayefanya maovu ni sawa na watu wanaosafiri kwenye<br />

meli. Wengine wako katika sehemu ya juu na wengine wako<br />

chini. Walioko chini hupata maji kutoka kwa walio juu, na<br />

kwa hiyo walikuwa wakiwasumbua sumbua (kwa kuwataka<br />

wawape maji kila wanapohitajia), hivyo waliamua kutoboa<br />

sehemu ya chini ya meli. Kisha wale wa juu waliwajia na<br />

kuwauliza, “Imekuwaje (mbona mnatoboa meli)?” Walijibu,<br />

“Mmetusumbua (na maji yenu) kwa hiyo tumeona hapana<br />

namna nyingine ya kupata maji ila kutoboa tundu yaingie.”<br />

Kama (wale wa juu) watawakataza wasiendelee na kitendo<br />

hicho (cha kutoboa meli) watakuwa wamewaokoa wale wa<br />

chini na kujiokoa wao wenyewe. Vinginevyo, wakiwaachia<br />

waendelee kutoboa watakuwa wamejiangamiza wao<br />

wenyewe pamoja na hao wenye kutoboa.” (Bukhari).<br />

Ugumu wa kusimamisha Uislamu katika Jamii<br />

uko wapi?<br />

Tumekwishaona umuhimu wa Uislamu kuyaongoza maisha<br />

ya binaadamu katika sura zake zote. Tumezingatia pia nini maana<br />

ya kusimamisha Uislamu katika jamii; lengo la kuletwa mitume<br />

duniani; na wajibu wetu wa kuhakikisha kuwa siku zote jamii<br />

inaongozwa na mafundisho yaliyoletwa na mitume wa Allah (s.w).<br />

lkiwa yote hayo tunayajua na kuyakubali, kwanini hatujaweza<br />

kuusimamisha Uislamu katika jamii yetu? Ugumu uko wapi.?<br />

Kushika mamlaka ya dola na kuyatumia hayo kutekeleza<br />

maamrisho ya Allah (s.w) ni kazi inayohitaji jitihada kubwa,<br />

kujitolea mali na nafsi kwa kiwango kikubwa sana na subira. Kwa<br />

sababu ya ugumu wa kazi yenyewe, baadhi yetu tumetafuta njia za<br />

mkato au nyepesi za kuikwepa kazi hiyo huku tukijidanganya kuwa<br />

tunaifanya kazi hiyo. Hivi sasa Waislamu tumegawanyika katika<br />

makundi makubwa matatu.<br />

26

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!