08.06.2013 Views

Download - islamic education panel

Download - islamic education panel

Download - islamic education panel

SHOW MORE
SHOW LESS

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

(6) Makabila ya Waarabu yatakuwa huru kufanya itifaki<br />

(urafiki) na upande wowote ule yanayoupendelea.<br />

(7) Pasiwe na vita kwa kipindi cha miaka 10 baina ya<br />

Waislamu na Maquraish na baina ya washirika (Allies) wa<br />

Waislamu na washirika wa Maquraish.<br />

(8) Hapana ruhusa ya kutengua hata shuruti moja katika hizi<br />

kabla ya miaka 10 kupita.<br />

Kwa ujumla Waislamu hawakufurahishwa na baadhi ya<br />

masharti ya mkataba hasa sharti la tano (5). Waliona kuwa<br />

wamedhalilishwa na kuonewa.<br />

Aidha Maquraish walionesha tabia ya dharau kwa Mtume<br />

(s.a.w), walikataa asitajwe kama Mtume wa Mwenyezi Mungu bali,<br />

itajwe kuwa ni mkataba baina ya Muhammad bin Abdillahi na<br />

Maquraish (waliwakilishwa na Suhail bin ‘Amr). Si hivyo tu, bali<br />

kabla hata mkataba haujatiwa sahihi alitokea Abu Jandal bin<br />

Suhail bin ‘Amr akakimbilia kwa Waislamu. Yeye alisilimu Makka<br />

na sasa anakimbia mateso. Suhail alimkamata na kumcharaza<br />

bakora kisha kumrudisha Makkah akaendelee kuteswa. Waislamu<br />

walimhurumia na kuomba asihusishwe na kifungu cha tano (5) cha<br />

mkataba lakini Suhail alikataa vinginevyo mkataba wa amani<br />

uvunjike. Mtume (s.a.w) alimsihi Abu Jandal afanye subira na<br />

arudi Makkah.<br />

Amani iliyopatikana baada ya mkataba wa Hudaibiya<br />

ilirahisisha maingiliano kati ya makafiri wa Makkah na Waislamu<br />

wa Madina. Kabla ya mkataba, Waislamu wa Madina na makafiri<br />

wa Makkah walikuwa na uhasama mkubwa. Hapakuwa na<br />

maingiliano ya kidugu wala kirafiki. Lakini baada ya mkataba huo<br />

watu wa Makkah walizuru Madinah kwa ajili ya biashara na<br />

kuwatembelea ndugu zao. Katika maingiliano haya Maquraysh<br />

walipata fursa ya kushuhudia ubora wa maisha ya jamii ya<br />

Kiislamu na walivutiwa sana na tabia na maadili ya Waislamu. Pia<br />

182

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!