Download - islamic education panel
Download - islamic education panel
Download - islamic education panel
Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
(6) Makabila ya Waarabu yatakuwa huru kufanya itifaki<br />
(urafiki) na upande wowote ule yanayoupendelea.<br />
(7) Pasiwe na vita kwa kipindi cha miaka 10 baina ya<br />
Waislamu na Maquraish na baina ya washirika (Allies) wa<br />
Waislamu na washirika wa Maquraish.<br />
(8) Hapana ruhusa ya kutengua hata shuruti moja katika hizi<br />
kabla ya miaka 10 kupita.<br />
Kwa ujumla Waislamu hawakufurahishwa na baadhi ya<br />
masharti ya mkataba hasa sharti la tano (5). Waliona kuwa<br />
wamedhalilishwa na kuonewa.<br />
Aidha Maquraish walionesha tabia ya dharau kwa Mtume<br />
(s.a.w), walikataa asitajwe kama Mtume wa Mwenyezi Mungu bali,<br />
itajwe kuwa ni mkataba baina ya Muhammad bin Abdillahi na<br />
Maquraish (waliwakilishwa na Suhail bin ‘Amr). Si hivyo tu, bali<br />
kabla hata mkataba haujatiwa sahihi alitokea Abu Jandal bin<br />
Suhail bin ‘Amr akakimbilia kwa Waislamu. Yeye alisilimu Makka<br />
na sasa anakimbia mateso. Suhail alimkamata na kumcharaza<br />
bakora kisha kumrudisha Makkah akaendelee kuteswa. Waislamu<br />
walimhurumia na kuomba asihusishwe na kifungu cha tano (5) cha<br />
mkataba lakini Suhail alikataa vinginevyo mkataba wa amani<br />
uvunjike. Mtume (s.a.w) alimsihi Abu Jandal afanye subira na<br />
arudi Makkah.<br />
Amani iliyopatikana baada ya mkataba wa Hudaibiya<br />
ilirahisisha maingiliano kati ya makafiri wa Makkah na Waislamu<br />
wa Madina. Kabla ya mkataba, Waislamu wa Madina na makafiri<br />
wa Makkah walikuwa na uhasama mkubwa. Hapakuwa na<br />
maingiliano ya kidugu wala kirafiki. Lakini baada ya mkataba huo<br />
watu wa Makkah walizuru Madinah kwa ajili ya biashara na<br />
kuwatembelea ndugu zao. Katika maingiliano haya Maquraysh<br />
walipata fursa ya kushuhudia ubora wa maisha ya jamii ya<br />
Kiislamu na walivutiwa sana na tabia na maadili ya Waislamu. Pia<br />
182