08.06.2013 Views

Download - islamic education panel

Download - islamic education panel

Download - islamic education panel

SHOW MORE
SHOW LESS

You also want an ePaper? Increase the reach of your titles

YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.

(ii) Kusengenyana, kudhaniana vibaya na<br />

kupekuana<br />

Kusengenya ni jambo ovu mno linalovuruga upendo na<br />

udugu katika kundi la Waislamu. Kusengenya ni kuongea juu ya<br />

ndugu yako yale ambayo asingaliyapendelea kuyasikia kama<br />

angelikuwepo, hata kama hayo yanayoongelewa ni ya kweli.<br />

Abu Hurairah amesimulia kuwa Mtume wa Allah aliuliza:<br />

Wote mnajua kusengenya ni nini? Walijibu (Waislamu)<br />

Allah na Mtume wake ndio wajuzi zaidi. Akasema:<br />

maongezi juu ya ndugu yako ambayo hayapendi. Aliulizwa:<br />

Je, kama kile kinachozungumzwa ni kweli juu ya ndugu<br />

yangu? Akajibu: Kama hilo unalomsengenya kwalo analo,<br />

bado utakuwa umesengenya, na kama hilo unalosema<br />

hanalo, basi utakuwa umemzulia. (Muislamu).<br />

Uislamu umekemea vikali kusengenya kama tunavyojifunza<br />

katika aya zifuatazo:<br />

Adhabu kali itamthubutikia kila mwenye kulamba kisogo,<br />

msengenyaji… (104:1)<br />

Enyi mlioamini! Jiepusheni sana na dhana (mbaya) kwani<br />

dhana ni dhambi. Wala msipeleleze (habari za watu). Wala<br />

baadhi yenu wasiwasengenye wengine. Je! Mmoja wenu<br />

anapenda kula nyama ya nduguye aliyekufa? La, hapendi.<br />

Na Mcheni Mwenyezi Mungu. Bila shaka Mwenyezi Mungu<br />

ni Mwenye kupokea toba, Mwingi wa kurehemu. (49:12)<br />

96

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!