08.06.2013 Views

Download - islamic education panel

Download - islamic education panel

Download - islamic education panel

SHOW MORE
SHOW LESS

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

nidhamu na kujiwekea ratiba ya kila siku kwa kuzingatia<br />

yafuatayo:<br />

1) Katika siku Muislamu ajiwekee saa moja hadi<br />

mbili za kujisomea Maarifa ya Uislamu.<br />

Wakati mzuri wa kujisomea ni baada ya kazi – baada ya<br />

swala ya Alasiri hadi Magharibi. Wakati mwingine mzuri wa<br />

kujisomea na kufanya Ibada nyingine uliosisitizwa katika Qur’an<br />

na Hadith za Mtume (s.a.w) ni theluthi ya mwisho ya usiku kati ya<br />

saa 8 na saa 11 alfajiri kwa kuwa katika muda huo kuna utulivu<br />

mkubwa kama Allah (s.w) anavyo tuarifu:-<br />

“Hakika kuamka usiku (na kufanya Ibada) kunawafikiana zaidi<br />

na moyo na maneno yanatuwa zaidi. Hakika mchana una<br />

shughuli nyingi” (73:6-7).<br />

Jambo muhimu kwa mwenye kuamka usiku kwa ajili ya<br />

kujisomea na kufanya Ibada nyingine ni kulala mapema mara tu<br />

baada ya swala ya Ishai.<br />

2) Kujitahidi kujiepusha na lagh-wi.<br />

Lagh-wi ni shughuli au jambo lolote lile lisilo mpelekea au<br />

linalomsahaulisha mja kuendea lengo la kuumbwa kwake na<br />

kusimamisha Uislamu katika jamii. Wenye akili ni wale wanaobakia<br />

na dhikri (kumzingatia) Allah (s.w)muda wote wa saa 24:<br />

202

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!