Download - islamic education panel
Download - islamic education panel
Download - islamic education panel
Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
Sifa za Mwanaharakati wa Kiislamu<br />
Zifuatazo ni sifa kuu anazostahiki kusifika kwazo Mwanahara<br />
kati wa Kiislamu:<br />
1. Ujuzi sahihi juu ya Uislamu<br />
2. Imani thabiti juu ya Uislamu<br />
3. Tabia njema (tabia ya utendaji)<br />
4. Kusimamisha Uislamu kuwa ndio lengo kuu la Maisha.<br />
5. Kutarajia malipo kutoka kwa Allah (s.w) tu.<br />
6. Kuwa na subira<br />
7. Kuwa na Hekima<br />
1. Ujuzi sahihi juu ya Uislamu<br />
Waislamu walio wengi wameridhika na Elimu ya Fiq-hi<br />
inayowawezesha kutekeleza Ibada maalum tu kama vile: Swala,<br />
Zakat, Swaumu, Hija, Ndoa, Talaka, Mirathi n.k. Kwa hiyo<br />
Waislamu walio wengi hawajui uchumi wa Kiislamu ukoje,<br />
mtazamo wa Uislamu juu ya siasa ni upi, Uislamu unautazamaje<br />
utamaduni n.k. Kwa ujumla Waislamu walio wengi hawana<br />
mtazamo sahihi wa Uislamu juu ya vipengele mbalimbali vya<br />
maisha ya jamii.Hivyo Mwanaharakati hana budi kuufahamu<br />
Uislamu kwa upana wake. Haina maana kuwa kila mtu anayetaka<br />
kulingania Uislamu katika jamii ni lazima awe amebobea<br />
kitaaluma katika kila kipengele muhimu cha maisha ya jamii ya<br />
Kiislamu bali hana budi kuwa na kiwango cha ujuzi<br />
kitakachomuwezesha kuishi Kiislamu katika kila kipengele cha<br />
maisha yake ya kibinafsi na yakijamii.<br />
Kwa maana nyingine ili kuhuisha Uislamu katika jamii na<br />
yapatikane mfanikio yanayotarajiwa Mwanaharakati hana budi kuwa<br />
na Elimu ya msingi juu ya:<br />
Lengo na Hadhi ya binaadamu hapa ulimwenguni<br />
Mtazamo wa Uislamu juu ya Elimu<br />
Mtazamo wa Uislamu juu ya Dini.<br />
64