Download - islamic education panel
Download - islamic education panel
Download - islamic education panel
Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
(Anasema Mwenyezi Mungu kuwaambia wanaadamu tangu<br />
hao wa zamani huko): Enyi wanaadamu! Hakika<br />
tumekuteremshieni nguo zifichazo tupu zenu na nguo za<br />
pambo; na nguo za utawa (yaani kumcha Mungu) ndizo<br />
bora”. Hayo ni katika ishara za (neema za) Mwenyezi<br />
Mungu ili wapate kukumbuka.(7:26)<br />
“Enyi wanaadamu. Shetani (Iblisi) asikutieni katika matata. Kama<br />
alivyowatoa wazee wenu katika Pepo; akawavua nguo zao ili<br />
kuwaonyesha tupu zao. Hakika yeye pamoja na kabila yake<br />
wanakuoneni, na hali ya kuwa hamuwaoni”. Bila shaka sisi<br />
tumewajaalia shetani kuwa marafiki kwa wale wasioamini. (7:27).<br />
Tukizingatia aya hizi kwa makini mambo yafuatayo<br />
yanajitokeza:<br />
Kwanza, Shetani alilaaniwa kwa sababu ya kukataa kutii<br />
amri ya Allah (s.w). Na alikataa kwa sababu alijidhani kuwa yu<br />
bora kuliko binaadam. Ubora huo aliuhusisha na kabila lake. Yaani<br />
yeye ni jinni na viumbe wa kabila la majini wameumbwa kwa moto<br />
na viumbe wa kabila la binadamu wameumbwa kwa udongo.<br />
Moto, alihisi iblisi, ni bora kuliko udongo, hivyo alikataa kutii<br />
amri ya Mola wake.<br />
Mtu kulitukuza kabila lake, au rangi yake, au nasaba yake au<br />
taifa lake na wakati huo huo kulibeza kabila, rangi, nasaba au taifa<br />
la mwenzake ni katika mwenendo wa shetani. Ni kibri kisichokuwa<br />
na msingi wowote na matokeo ya fikra hizi za kishetani yamekuwa<br />
ni chuki, bughudha na umwagaji damu usiokwisha katika dunia.<br />
Watu wengi wamedhulumiwa na wanaendelea kuteseka na hata<br />
164