Download - islamic education panel
Download - islamic education panel
Download - islamic education panel
Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
Sura ya Sita<br />
MIPANGO KATIKA HARAKATI ZA KIISLAMU<br />
Maana ya Mipango (Planning)<br />
Tunaweza kusema mipango ni utaratibu wa kuendea lengo<br />
husika kwa ufanisi kwa kufuata hatua baada ya hatua. Kuweka<br />
mipango ni kutengeneza njia ya kumfikisha mtu mahali<br />
anapokusudia kwenda kwa wepesi. Ukiwa njiani kuelekea<br />
uendako, waweza kupotea njia na kuelekea usikokusudia au<br />
waweza kufika mahali ukadhani umefika kumbe bado kutokana na<br />
kutokuwa na mpango wa safari.<br />
Umuhimu wa kuweka mipango<br />
Wataalamu wa fani ya mipango wana msemo “Ikiwa<br />
unashindwa kupanga, basi unapanga kushindwa”. maana yake ni<br />
kwamba ukishindwa kuweka mipango ya jambo lolote<br />
unalokusudia kulifanya, umeamua kushindwa kufanya jambo hilo.<br />
Hekima ya msemo huu ni kuwa, iwapo utafanya mambo bila ya<br />
kuweka mipango madhubuti, waweza kupoteza nguvu bure bila ya<br />
kupata matunda tarajiwa. Lakini endapo utapanga mipango yako<br />
vyema kabla ya kujitosa katika utekelezaji, kwanza utabakia katika<br />
lengo na pili hutafuja juhudi na nguvu zako katika mambo ambayo<br />
hayako katika mpango wako.<br />
Kwa muhutasari tunaona kuwa kuweka mipango katika<br />
kufanya mambo yetu ni muhimu kwa sababu zifuatazo:<br />
Kwanza, kuweka mipango hutufanya tuwe makini katika<br />
kuweka malengo. Kwa kuwa na mipango tutahakikisha kuwa<br />
tunaweka malengo yanayotekelezeka. Lengo lolote tunaloliweka ni<br />
lazima tuliweke kwenye mizani ya kiutekelezaji na tukiona<br />
halitekelezeki tunaliacha.<br />
169