08.06.2013 Views

Download - islamic education panel

Download - islamic education panel

Download - islamic education panel

SHOW MORE
SHOW LESS

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

Sura ya Sita<br />

MIPANGO KATIKA HARAKATI ZA KIISLAMU<br />

Maana ya Mipango (Planning)<br />

Tunaweza kusema mipango ni utaratibu wa kuendea lengo<br />

husika kwa ufanisi kwa kufuata hatua baada ya hatua. Kuweka<br />

mipango ni kutengeneza njia ya kumfikisha mtu mahali<br />

anapokusudia kwenda kwa wepesi. Ukiwa njiani kuelekea<br />

uendako, waweza kupotea njia na kuelekea usikokusudia au<br />

waweza kufika mahali ukadhani umefika kumbe bado kutokana na<br />

kutokuwa na mpango wa safari.<br />

Umuhimu wa kuweka mipango<br />

Wataalamu wa fani ya mipango wana msemo “Ikiwa<br />

unashindwa kupanga, basi unapanga kushindwa”. maana yake ni<br />

kwamba ukishindwa kuweka mipango ya jambo lolote<br />

unalokusudia kulifanya, umeamua kushindwa kufanya jambo hilo.<br />

Hekima ya msemo huu ni kuwa, iwapo utafanya mambo bila ya<br />

kuweka mipango madhubuti, waweza kupoteza nguvu bure bila ya<br />

kupata matunda tarajiwa. Lakini endapo utapanga mipango yako<br />

vyema kabla ya kujitosa katika utekelezaji, kwanza utabakia katika<br />

lengo na pili hutafuja juhudi na nguvu zako katika mambo ambayo<br />

hayako katika mpango wako.<br />

Kwa muhutasari tunaona kuwa kuweka mipango katika<br />

kufanya mambo yetu ni muhimu kwa sababu zifuatazo:<br />

Kwanza, kuweka mipango hutufanya tuwe makini katika<br />

kuweka malengo. Kwa kuwa na mipango tutahakikisha kuwa<br />

tunaweka malengo yanayotekelezeka. Lengo lolote tunaloliweka ni<br />

lazima tuliweke kwenye mizani ya kiutekelezaji na tukiona<br />

halitekelezeki tunaliacha.<br />

169

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!