08.06.2013 Views

Download - islamic education panel

Download - islamic education panel

Download - islamic education panel

SHOW MORE
SHOW LESS

You also want an ePaper? Increase the reach of your titles

YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.

(vii) Subira<br />

Kiongozi katika dola ya Kiislamu anatakiwa awe mwenye<br />

subira, mvumilivu na mstahimilivu. Kiongozi atekeleze wajibu<br />

wake ipasavyo na asitarajie kupendwa na kufurahiwa na watu<br />

wote. Waumini wa kweli tu ndio watakaomfurahia na kumsaidia<br />

atakapowaongoza kwa mujibu wa Qur-an na Sunnah. Lakini<br />

wanafiki, wenye husuda, wapenda vyeo na sifa na maadui wote wa<br />

Uislamu hawawezi kamwe kumfurahia kiongozi wa Kiislamu<br />

muadilifu. Kiongozi wa Kiislamu hana budi kukumbuka kuwa<br />

anafanya kazi ile ile ya Mtume (s.a.w). Arejee historia ajikumbushe<br />

maudhi na vitimbi vya kila namna alivyofanyiwa Mtume wa Allah<br />

na makafiri wa Makkah na Mayahudi na Wanafiki wa Madina.<br />

Kisha katika uongozi wake anapokumbana na matatizo ya<br />

kutukanwa, kusingiziwa, kupuuzwa n.k. ajiulize: “Je haya<br />

yaliyonifika yanaweza kulinganishwa na yale yaliyomfika Mtume<br />

wa Allah” Pia kiongozi wa Kiislamu anayejitahidi kutekeleza<br />

wajibu wake kwa mujibu wa Qur-an na Sunnah, hana budi<br />

kukumbuka kuwa malipo ya kazi yake yapo kwa Allah (s.w) na<br />

ndiye pekee anayewajibika kumuogopa na kutaka radhi yake.<br />

(viii) Uoni wa mbali<br />

Kiongozi ni lazima awe na mtazamo wa mbali, ajue<br />

anakoipeleka jamii ya Waislamu na aweze kubuni program za<br />

kuifikisha jamii huko. Hapa tunakusudia kuwa kiongozi wa<br />

Kiislamu awe na lengo la kusimamisha Uislamu katika jamii au<br />

ajue namna ya kulifikia lengo hilo. Hii ni pamoja na kuweza<br />

kutambua vikwazo na hatari zilizo mbele yao na kubuni mbinu na<br />

program za kukabiliana nazo.<br />

(ix) Uwezo wa Kubuni Mipango<br />

Kiongozi wa Kiislamu awe na uwezo wa kubuni mipango<br />

inayotekelezeka na mbinu bora za kufikia yale anayoyaona mbele.<br />

(x) Uwezo wa Kuunganisha Nguvu Kazi<br />

Kiongozi wa Kiislamu anatakiwa awe na uwezo wa<br />

kuunganisha nguvu kazi na yale yote yanayohitajika kufanikisha<br />

196

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!