08.06.2013 Views

Download - islamic education panel

Download - islamic education panel

Download - islamic education panel

SHOW MORE
SHOW LESS

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

Mwanaharakati atakapojiingiza katika kazi hii ya Mitume<br />

kwa matarajio ya kupata maslahi ya kidunia, kamwe asitarajie<br />

kufikia lengo la kuusimamisha Uislam katika jamii.<br />

6. Kuwa na Subira<br />

Subira ni kipengele cha tabia njema chenye maana pana.<br />

Hapa tutaona miongoni mwa maeneo ya subira anayotarajiwa<br />

kuyapitia mwanaharakati:<br />

(i) Kutokuwa na haraka katika kutoa maamuzi.<br />

Mwanaharakati anatakiwa anapopata jambo asilitolee uamuzi<br />

haraka haraka kabla ya kufikiri vya kutosha na kupata ushauri wa<br />

kutosha kutoka kwa watu anaowategemea kwa ujuzi wao na<br />

uadilifu wao. Uamuzi wa jazba hautakikani katika harakati za<br />

kuhuisha na kusimamisha Uislamu katika jamii.<br />

(ii) Kutokuwa na haraka ya kupata matunda ya<br />

harakati. Mwanaharakati asiwe na haraka ya kutaka kuona<br />

mabadiliko ya haraka haraka katika jamii kutokana na kazi yake.<br />

Anatakiwa kuifanya kazi hii kwa muda wote wa maisha yake kwa<br />

lengo la kuusimamisha Uislamu bila ya kukatishwa tamaa na<br />

chochote. Mwanaharakati bila ya kuwa na msimamo huu, kazi hii<br />

itamshinda na atakuwa miongoni mwa waliokata tamaa na Rehma<br />

ya Allah (s.w).<br />

.....<br />

“...... wala msikate tamaa na Rehema ya Mwenyezi Mungu<br />

Na hawakati tamaa na rehma ya Mwenyezi Mungu<br />

isipokuwa makafiri”.(12:87)<br />

(iii) Ni katika subira vile vile mtu kubakia na uamuzi<br />

wake mwema mpaka hatua ya mwisho. Mwanaharakati<br />

anatakiwa awe na msimamo thabiti katika kazi yake hii ya<br />

72

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!