Download - islamic education panel
Download - islamic education panel
Download - islamic education panel
Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
Mwanaharakati atakapojiingiza katika kazi hii ya Mitume<br />
kwa matarajio ya kupata maslahi ya kidunia, kamwe asitarajie<br />
kufikia lengo la kuusimamisha Uislam katika jamii.<br />
6. Kuwa na Subira<br />
Subira ni kipengele cha tabia njema chenye maana pana.<br />
Hapa tutaona miongoni mwa maeneo ya subira anayotarajiwa<br />
kuyapitia mwanaharakati:<br />
(i) Kutokuwa na haraka katika kutoa maamuzi.<br />
Mwanaharakati anatakiwa anapopata jambo asilitolee uamuzi<br />
haraka haraka kabla ya kufikiri vya kutosha na kupata ushauri wa<br />
kutosha kutoka kwa watu anaowategemea kwa ujuzi wao na<br />
uadilifu wao. Uamuzi wa jazba hautakikani katika harakati za<br />
kuhuisha na kusimamisha Uislamu katika jamii.<br />
(ii) Kutokuwa na haraka ya kupata matunda ya<br />
harakati. Mwanaharakati asiwe na haraka ya kutaka kuona<br />
mabadiliko ya haraka haraka katika jamii kutokana na kazi yake.<br />
Anatakiwa kuifanya kazi hii kwa muda wote wa maisha yake kwa<br />
lengo la kuusimamisha Uislamu bila ya kukatishwa tamaa na<br />
chochote. Mwanaharakati bila ya kuwa na msimamo huu, kazi hii<br />
itamshinda na atakuwa miongoni mwa waliokata tamaa na Rehma<br />
ya Allah (s.w).<br />
.....<br />
“...... wala msikate tamaa na Rehema ya Mwenyezi Mungu<br />
Na hawakati tamaa na rehma ya Mwenyezi Mungu<br />
isipokuwa makafiri”.(12:87)<br />
(iii) Ni katika subira vile vile mtu kubakia na uamuzi<br />
wake mwema mpaka hatua ya mwisho. Mwanaharakati<br />
anatakiwa awe na msimamo thabiti katika kazi yake hii ya<br />
72