Download - islamic education panel
Download - islamic education panel
Download - islamic education panel
Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
Sura ya Nne<br />
KUNDI LA HARAKATI ZA KIISLAMU<br />
Ni lipi kundi la Harakati<br />
Kundi la Harakati ni kundi lililo anzishwa na wanaharakati<br />
kwa lengo la kulingania na kusimamisha Uislamu katika jamii.<br />
Umuhimu wa kuwepo Kundi la Harakati<br />
Kila Muislamu lazima afahamu kuwa, hakuna Uislamu wa mtu<br />
binafsi. Kama Uislamu haujasimamishwa katika jamii mtu mmoja<br />
mmoja hawezi kuufuata Uislamu katika kukiendea kila kipengele<br />
cha maisha yaki kibinafsi na kijamii kama anavyoagiza Allah (s.w):<br />
“Enyi mlioamini! Ingieni katika Uislamu wote (kwa kufuata<br />
hukumu zote) wala msifuate nyayo za Sheitwan, kwa hakika<br />
yeye kwenu ni Adui dhahiri” (2:208)<br />
Mtu mmoja hawezi kuuingia Uislamu wote kwa sababu kuna<br />
vipengele vingi vya kijamii ambavyo mtu binafsi hawezi kuvitekeleza<br />
kwa kufuata mwongozo wa Qur-an na Sunnah, bali inabidi afuate<br />
nyayo za Shetani kwa kufuata utaratibu wa maisha uliowekwa na<br />
“matwaghuti” au wachupaji mipaka ya Allah (s.w). Kwa mfano, katika<br />
miongozo ya “Kitwaghuti” uchumi umejengwa juu ya misingi ya riba,<br />
kamari, ulevi, hongo, ulaghai, dhulma, ulanguzi, n.k. Waislamu binafsi<br />
wanaoishi katika jamii hizo hawana namna ya kujivua na uchumi huo<br />
haramu wakiwa katika hali ya mtu mmoja mmoja na kwa vyovyote vile<br />
kipato chao kwa njia moja au nyingine kitatokana na Riba, Kamari,<br />
81