08.06.2013 Views

Download - islamic education panel

Download - islamic education panel

Download - islamic education panel

SHOW MORE
SHOW LESS

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

Sura ya Nne<br />

KUNDI LA HARAKATI ZA KIISLAMU<br />

Ni lipi kundi la Harakati<br />

Kundi la Harakati ni kundi lililo anzishwa na wanaharakati<br />

kwa lengo la kulingania na kusimamisha Uislamu katika jamii.<br />

Umuhimu wa kuwepo Kundi la Harakati<br />

Kila Muislamu lazima afahamu kuwa, hakuna Uislamu wa mtu<br />

binafsi. Kama Uislamu haujasimamishwa katika jamii mtu mmoja<br />

mmoja hawezi kuufuata Uislamu katika kukiendea kila kipengele<br />

cha maisha yaki kibinafsi na kijamii kama anavyoagiza Allah (s.w):<br />

“Enyi mlioamini! Ingieni katika Uislamu wote (kwa kufuata<br />

hukumu zote) wala msifuate nyayo za Sheitwan, kwa hakika<br />

yeye kwenu ni Adui dhahiri” (2:208)<br />

Mtu mmoja hawezi kuuingia Uislamu wote kwa sababu kuna<br />

vipengele vingi vya kijamii ambavyo mtu binafsi hawezi kuvitekeleza<br />

kwa kufuata mwongozo wa Qur-an na Sunnah, bali inabidi afuate<br />

nyayo za Shetani kwa kufuata utaratibu wa maisha uliowekwa na<br />

“matwaghuti” au wachupaji mipaka ya Allah (s.w). Kwa mfano, katika<br />

miongozo ya “Kitwaghuti” uchumi umejengwa juu ya misingi ya riba,<br />

kamari, ulevi, hongo, ulaghai, dhulma, ulanguzi, n.k. Waislamu binafsi<br />

wanaoishi katika jamii hizo hawana namna ya kujivua na uchumi huo<br />

haramu wakiwa katika hali ya mtu mmoja mmoja na kwa vyovyote vile<br />

kipato chao kwa njia moja au nyingine kitatokana na Riba, Kamari,<br />

81

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!