Download - islamic education panel
Download - islamic education panel
Download - islamic education panel
Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
Kwa mfano mipango ya Kistratejia kwa Waislamu wa<br />
Tanzania sasa ni kuwaelimisha Waislamu ili (a) Waujue Uislamu<br />
kwamba ndio mfumo pekee sahihi wa maisha wanaopaswa<br />
kuufuata. (b) Kuijua hadhi yao kama Makhalifa wa Allah (s.w)<br />
hapa ardhini. (c) Waweze kujenga na kuendesha taasisi muhimu<br />
za Kiislamu, kusimamia elimu, uchumi, maadili na masuala mbali<br />
mbali ya kijamii. (d) Waweze kushikamana na kuwa tayari kujitoa<br />
muhanga kuupigania Uislamu kwa mali na nafsi zao.<br />
Kwa kuwa na mpango wa Kistratejia Waislamu wanatakiwa:<br />
Kwanza kushikamana wote katika kuendea mpango huo.<br />
Hata kama itakuwepo tofauti ndogo ndogo miongoni mwao au<br />
miongoni mwa jumuiya na taasisi zao, wasiruhusu vivunje<br />
mshikamano wao katika kuendea lengo hili.<br />
Pili, wasipoteze rasilimali zao ikiwa ni akili zao, nguvu zao<br />
na mali zao katika jambo lisilowapeleka katika mpango huu wa<br />
Kistratejia.<br />
Tatu, wasikubali kutolewa katika agenda yao. Mara nyingi<br />
maadui wamekuwa wakiwachezea Waislamu kwa kuwaletea<br />
agenda ambazo zinawashughulisha badala ya kutizama mipango<br />
yao. Kwa mfano wanaweza kuja na agenda ya kuwa na Kadhi,<br />
Waislamu wakapoteza muda kulumbana juu ya umuhimu wa kuwa<br />
na Kadhi na nani awe Kadhi. Inapotokea jambo kama hilo,<br />
Waislamu wanatakiwa wajiulize je, linawasaidiaje kukamilika kwa<br />
mpango wao wa kistratejia. Kama haliwasaidii lolote, waliache<br />
kama lilivyo na waunde kikundi cha watu wachache<br />
kulishughulikia, huku nguvu kubwa ikiendelea na mpango uliopo.<br />
Nne, wawe tayari kusamehe au kutoa sadaka baadhi ya haki,<br />
maslahi na fursa zao kwa ajili ya manufaa makubwa ya lengo lao la<br />
kistratejia.<br />
180