Download - islamic education panel
Download - islamic education panel
Download - islamic education panel
Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
Hongo, Dhulma, Ulevi, n.k. Huo ni mfano mmoja tu wa uchumi, kuna<br />
masuala ya Sheria na Hukumu za Kijahili, Utamaduni wa Kijahili,<br />
Siasa za Kitwaghuti na mifumo mingine ya Kitwaghuti katika kila fani<br />
ya maisha ya jamii.<br />
Kutokana na hali hii ipo haja ya kuusimamisha Uislamu<br />
katika jamii ili kuwawezesha Waislamu kukiendea kila kipengele<br />
cha maisha ya kibinafsi na kijamii kwa kufuata baraabara<br />
muongozo wa Qur-an na Sunnah.<br />
Kazi ya kusimamisha Uislamu katika jamii haiwezi kamwe<br />
kufanikishwa na nguvu ya mtu mmoja mmoja. Mitume wa Allah<br />
(s.w) hawakuweza wao wenyewe kufanikisha mpaka walipopata<br />
wafuasi waliosaidiana nao bega kwa bega. Hivyo jukumu la<br />
kuusimamisha na kuuendeleza Uislamu liko juu ya mabega ya<br />
waumini wote katika jamii.<br />
Waislamu wataweza kutekeleza jukumu hili endapo tu<br />
watakuwa wameungana pamoja na kuwa umma mmoja au endapo<br />
tu watatekeleza amri ya Allah (s.w) ifuatayo:<br />
....................<br />
“Na shikamaneni kwa kamba (dini) ya Allah nyote wala<br />
msifarikiane…” (3:103)<br />
Bila shaka Waislamu wakitekeleza hili watakuwa umma<br />
wenye nguvu na uwezo wa kusimamisha Uislamu katika jamii<br />
kama Allah (s.w) anavyotuthibitishia:<br />
..................<br />
“Nyinyi ndio umma bora kuliko umma zote<br />
zilizodhihirishiwa watu (ulimwenguni) mnaamrisha yaliyo<br />
mema na mnakataza yaliyo maovu na mnamwamini<br />
Mwenyezi Mungu...........” (3:110)<br />
82