08.06.2013 Views

Download - islamic education panel

Download - islamic education panel

Download - islamic education panel

SHOW MORE
SHOW LESS

You also want an ePaper? Increase the reach of your titles

YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.

Al-Amin. Wakubwa na wadogo walimheshimu na walimpa amana<br />

zao kuwawekea hata baada ya kupewa Utume. Tabia yake njema<br />

isiyo na mfano wake katika jamii yake ni uthibitisho kuwa Mutme<br />

(s.a.w) aliandaliwa ki-il-hamu kabla hajapewa utume.<br />

Tabia yake njema isiyo na mfano wake kuanzia utotoni hadi<br />

utuuzima wake inaashiria wazi kuwa hakuwa zao la jamii yake, bali<br />

aliandaliwa na Mola wake awe vile ili awe kiigizo chema kwa watu<br />

wa Umma wake.<br />

(v) Ndoa yake na Bibi Khadija<br />

Umaarufu wa Muhammad (s.a.w) kutokana na tabia yake<br />

tukufu ulienea Bara Arab nzima. Bibi Khadijah, mwanamke mjane<br />

miongoni kwa matajiri wakubwa wa Makkah, alivutiwa na tabia ya<br />

Muhammad (s.a.w). Bibi Khadijah alimtaka Muhammad<br />

ampelekee bidhaa zake Yemen kwa ujira wa ngamia wawili.<br />

Muhammad (s.a.w) alikubali na alirejea na faida kubwa zaidi<br />

kuliko matazamio ya Bibi Khadijah. Bibi Khadijah alivutika kwa<br />

faida hiyo kubwa na ikambidi tena amuombe Muhammad (s.a.w)<br />

ampelekee bidhaa zake Sham(Syria)kwa malipo ya ngamia wanne.<br />

Katika msafara huu, Muhammad (s.a.w) alimletea Bibi Khadijah<br />

faida kubwa zaidi ya mategemeo yake. Khadijah alikuwa hajawahi<br />

kupata faida kubwa kiasi kile tangu aanze kufanya biashara katika<br />

misafara ya Sham. Pamoja na furaha ya kupata faida kubwa kiasi<br />

hicho, Bibi Khadija alizidi kufurahi na kuvutiwa na Muhammad<br />

aliposikia sifa zake za ajabu kutokana na taarifa ya mtumishi wake<br />

Maisarah waliyeongozana naye. Kutokana na alivyovutika Bibi<br />

Khadijah hakuweza kustahamili kukaa mbali na Muhammad<br />

(s.a w) Hivyo alimtaka radhi Muhammad na kuomba amuoe. Bibi<br />

Khadijah wakati huo alikuwa mjane mwenye umri wa miaka 40,<br />

aliyewahi kuolewa mara mbili na kujaaliwa kupata watoto watatu<br />

– wawili wanaume na mmoja mwanamke. Kabla ya hapo matajiri<br />

na machifu wengi wa Makkah walipeleka posa zao kwa Bibi<br />

45

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!