Download - islamic education panel
Download - islamic education panel
Download - islamic education panel
You also want an ePaper? Increase the reach of your titles
YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.
Al-Amin. Wakubwa na wadogo walimheshimu na walimpa amana<br />
zao kuwawekea hata baada ya kupewa Utume. Tabia yake njema<br />
isiyo na mfano wake katika jamii yake ni uthibitisho kuwa Mutme<br />
(s.a.w) aliandaliwa ki-il-hamu kabla hajapewa utume.<br />
Tabia yake njema isiyo na mfano wake kuanzia utotoni hadi<br />
utuuzima wake inaashiria wazi kuwa hakuwa zao la jamii yake, bali<br />
aliandaliwa na Mola wake awe vile ili awe kiigizo chema kwa watu<br />
wa Umma wake.<br />
(v) Ndoa yake na Bibi Khadija<br />
Umaarufu wa Muhammad (s.a.w) kutokana na tabia yake<br />
tukufu ulienea Bara Arab nzima. Bibi Khadijah, mwanamke mjane<br />
miongoni kwa matajiri wakubwa wa Makkah, alivutiwa na tabia ya<br />
Muhammad (s.a.w). Bibi Khadijah alimtaka Muhammad<br />
ampelekee bidhaa zake Yemen kwa ujira wa ngamia wawili.<br />
Muhammad (s.a.w) alikubali na alirejea na faida kubwa zaidi<br />
kuliko matazamio ya Bibi Khadijah. Bibi Khadijah alivutika kwa<br />
faida hiyo kubwa na ikambidi tena amuombe Muhammad (s.a.w)<br />
ampelekee bidhaa zake Sham(Syria)kwa malipo ya ngamia wanne.<br />
Katika msafara huu, Muhammad (s.a.w) alimletea Bibi Khadijah<br />
faida kubwa zaidi ya mategemeo yake. Khadijah alikuwa hajawahi<br />
kupata faida kubwa kiasi kile tangu aanze kufanya biashara katika<br />
misafara ya Sham. Pamoja na furaha ya kupata faida kubwa kiasi<br />
hicho, Bibi Khadija alizidi kufurahi na kuvutiwa na Muhammad<br />
aliposikia sifa zake za ajabu kutokana na taarifa ya mtumishi wake<br />
Maisarah waliyeongozana naye. Kutokana na alivyovutika Bibi<br />
Khadijah hakuweza kustahamili kukaa mbali na Muhammad<br />
(s.a w) Hivyo alimtaka radhi Muhammad na kuomba amuoe. Bibi<br />
Khadijah wakati huo alikuwa mjane mwenye umri wa miaka 40,<br />
aliyewahi kuolewa mara mbili na kujaaliwa kupata watoto watatu<br />
– wawili wanaume na mmoja mwanamke. Kabla ya hapo matajiri<br />
na machifu wengi wa Makkah walipeleka posa zao kwa Bibi<br />
45