Download - islamic education panel
Download - islamic education panel
Download - islamic education panel
Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
Kufikia mwaka 1970 wakaanzisha mradi mkubwa waliouita<br />
“Islam in Africa Project” yaani “Mradi wa kuua Uislamu<br />
Afrika” na Mkurugenzi wake mkuu akawa Nairobi, Kenya. Mradi<br />
huu kwanza ulifanya kazi ya kuwatafiti Waislamu na udhaifu wao<br />
iIi kujua namna ya kuwamaliza. Wakagundua kuwa udhaifu<br />
mkubwa wa Waislamu ni:<br />
(i) Kutojua Uislamu wao na kutofuata Qur’an na Sunnah.<br />
(ii) Kuridhika na kukaa mijini tu na kutofanya Da’awah<br />
vijijini.<br />
Wao, Wakristo, wakaingia vijijini na kueneza Ukristo. Hivyo<br />
Uislamu ambao ulikuja Afrika Mashariki tangu karne ya tisa, leo<br />
unashindana na hata kuzidiwa nguvu na Ukristo uliokuja Afrika<br />
Mashariki miaka elfu baadaye.<br />
Mbinu kubwa iliyopangwa na kutumiwa Afrika ilikuwa<br />
kuwaelekeza Mapadri wote wajisingizie kuwa ni marafiki wa<br />
Waislamu. “Wote ni ndugu.” Halafu bila kuwagutua Waislamu,<br />
waeneze mafundisho ya Ukristo polepole kwa Waislamu hasa kwa<br />
kupitia shule na hospitali. Lengo lilikuwa ni kuwafanya Waislamu<br />
waritadi.<br />
Kampeni hiyo imefikia hatua kubwa sana hivi leo kiasi<br />
ambacho Waislamu bila hata kujijua wanawafuata Wakristo katika<br />
mambo mengi. Zimezuka siku hizi “Ibada” za pamoja za<br />
madhehebu yote. Yaani Waislamu na Wakristo wanashirikiana<br />
Ibada kuombea kitu fulani, Waislamu wanaume na wanawake<br />
wanavaa kama Wakristo,huna namna ya kumjua yupi Muislamu<br />
na yupi Mkristo. Hivyo huwezi kujua yupi umtolee “Assalaam<br />
Alaykum”. Katika harusi ndio kabisa. Binti wa Kiislamu anakuwa<br />
kama Mkristo halisi. Leo mpaka katika mazishi utakuta Waislamu<br />
wanamweka hadharani maiti mwenzao Muislamu na kuwaalika<br />
watu wote waliokusanyika hapo wake kwa waume waje,<br />
145