08.06.2013 Views

Download - islamic education panel

Download - islamic education panel

Download - islamic education panel

SHOW MORE
SHOW LESS

You also want an ePaper? Increase the reach of your titles

YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.

(iii) Kuchangamkiana<br />

Kuchangamkiana kila mnapokutana ni jambo linalopalilia<br />

udugu na upendo nyoyoni mwa Waislamu. Jambo hili linatiliwa<br />

mkazo na Hadith ifuatayo:<br />

Jabir (r.a) ameeleza kuwa Mtume wa Allah amesema: “Kila<br />

kitendo kizuri ni sadaqa, na ni miongoni mwa kitendo chema<br />

kuwa unakutana na ndugu yako (Muislamu) kwa uso<br />

mchangamfu, na kwamba unamimina kutoka kwenye ndoo<br />

yako kwa ndoo ya ndugu yako”. (Ahmed, Tirmiz).<br />

(iv) Kupeana zawadi<br />

Kupeana zawadi mara kwa mara ni jambo linalojenga udugu<br />

na upendo nyoyoni mwa Waislamu. Umuhimu wa kupeana zawadi<br />

unabainika katika Hadithi ifuatayo:-<br />

Aysha (r.a) amesimulia kuwa Mtume wa Allah amesema:<br />

“Peaneni zawadi kwani zawadi inaondoa chuki”. (Tirmidh)<br />

(v) Kusuluhishana<br />

Waislamu wanapoingiliwa na Shetani wakagombana, mara<br />

baada ya kutulia, wanalazimika wasuluhishane na kusameheana.<br />

Kila wakati Waislamu wanatakiwa wawe katika upendo na amani<br />

kama Hadithi ifuatayo inavyosisitiza:<br />

Abu Hurairah (r.a) amesema kuwa Mtume wa Allah<br />

amesema:“Hamtaingia Peponi mpaka muamini; na<br />

hamtakuwa wenye kuamini mpaka mpendane. Je,<br />

nisikufahamisheni jambo ambalo mkilifanya mtaweza<br />

kupendana? Enezeni (dumisheni) amani miongoni mwenu.<br />

(Muslim).<br />

Kwa mujibu wa mafundisho ya Mtume (s.a.w) Waislamu<br />

hawaruhusiwi kununiana kiasi cha kutotoleana salaam kwa zaidi<br />

ya siku tatu.<br />

90

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!