Download - islamic education panel
Download - islamic education panel
Download - islamic education panel
You also want an ePaper? Increase the reach of your titles
YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.
(iii) Kuchangamkiana<br />
Kuchangamkiana kila mnapokutana ni jambo linalopalilia<br />
udugu na upendo nyoyoni mwa Waislamu. Jambo hili linatiliwa<br />
mkazo na Hadith ifuatayo:<br />
Jabir (r.a) ameeleza kuwa Mtume wa Allah amesema: “Kila<br />
kitendo kizuri ni sadaqa, na ni miongoni mwa kitendo chema<br />
kuwa unakutana na ndugu yako (Muislamu) kwa uso<br />
mchangamfu, na kwamba unamimina kutoka kwenye ndoo<br />
yako kwa ndoo ya ndugu yako”. (Ahmed, Tirmiz).<br />
(iv) Kupeana zawadi<br />
Kupeana zawadi mara kwa mara ni jambo linalojenga udugu<br />
na upendo nyoyoni mwa Waislamu. Umuhimu wa kupeana zawadi<br />
unabainika katika Hadithi ifuatayo:-<br />
Aysha (r.a) amesimulia kuwa Mtume wa Allah amesema:<br />
“Peaneni zawadi kwani zawadi inaondoa chuki”. (Tirmidh)<br />
(v) Kusuluhishana<br />
Waislamu wanapoingiliwa na Shetani wakagombana, mara<br />
baada ya kutulia, wanalazimika wasuluhishane na kusameheana.<br />
Kila wakati Waislamu wanatakiwa wawe katika upendo na amani<br />
kama Hadithi ifuatayo inavyosisitiza:<br />
Abu Hurairah (r.a) amesema kuwa Mtume wa Allah<br />
amesema:“Hamtaingia Peponi mpaka muamini; na<br />
hamtakuwa wenye kuamini mpaka mpendane. Je,<br />
nisikufahamisheni jambo ambalo mkilifanya mtaweza<br />
kupendana? Enezeni (dumisheni) amani miongoni mwenu.<br />
(Muslim).<br />
Kwa mujibu wa mafundisho ya Mtume (s.a.w) Waislamu<br />
hawaruhusiwi kununiana kiasi cha kutotoleana salaam kwa zaidi<br />
ya siku tatu.<br />
90