Download - islamic education panel
Download - islamic education panel
Download - islamic education panel
Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
5. Kulingania kwa Mawaidha mazuri<br />
Kwa mnasaba wa kulingania Uislamu kwa lengo la<br />
kuusimamisha katika jamii, mawaidha mazuri ni yale yaliyobeba<br />
sifa zifuatazo:<br />
(i) Yanayotokana na ujumbe halisi wa Qur’an na Sunnah.<br />
Yasiwe yale yanayotokana na simulizi za watu. Yaani<br />
usiwe ni ujumbe wa mapokeo. Kwa maana nyingine<br />
yasitoke kwa sheikh au mwanazuoni fulani bali<br />
yashehenezwe na ushahidi wa Qur’an na Hadith sahihi<br />
za Mtume (s.a.w) na hasa ukizingatia kuwa wahyi<br />
kwa njia ya Jibril umekomea kwa Mtume (s.a.w).<br />
Kwahiyo kila muumini wa kweli ana fursa ya kutumia<br />
vipawa alivyopewa katika kuipambanua Qur’an na<br />
Hadith ili aweze kuitekeleza vilivyo.<br />
(ii) Yale yanayowezesha kuitambua nafasi au hadhi ya<br />
Muislamu katika jamii na kulitambua fika lengo la<br />
kuumbwa binaadamu.<br />
(iii)Yanayo mjenga Muislamu na kumpa ari na hamasa ya<br />
kuufuata Uislamu katika kukiendea kila kipengele cha<br />
maisha yake ya kibinafsi na kumpa ari na hamasa ya<br />
kufanya jitihada za makusudi za kusimamisha Uislamu<br />
katika jamii.<br />
(iv) Yanayomuwezesha mtu kuwa na mtazamo sahihi wa<br />
Uislamu juu ya dhana mbali mbali za maisha ya<br />
kibinafsi na kijamii. Yaani mawaidha mazuri ni yale<br />
yanaonesha mtazamo sahihi kwa mujibu wa Qur’an na<br />
Hadith sahihi, juu ya elimu, dini, imani, uchumi,siasa,<br />
utamaduni n.k.<br />
(v) Yaliyoepukana na laghawi. Yaani mawaidha mazuri ni<br />
yale yaliyoepukana na porojo au hadithi za “paukwa<br />
pakawa”, ambazo huwafanya watu waishie kwenye<br />
kuangua vicheko bila ya kuondoka na ujumbe<br />
wowote utakao pelekea kuongeza ufanisi katika<br />
kuufuata Uislamu kibinafsi na kijamii.<br />
129