08.06.2013 Views

Download - islamic education panel

Download - islamic education panel

Download - islamic education panel

SHOW MORE
SHOW LESS

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

Mkataba wa Hudaibiya unatoa ufafanuzi na mafunzo<br />

makubwa juu ya nukta hizi.<br />

Mkataba wa Hudaibiya<br />

(Dhul-Qa’dah 6, A.H/March 628)<br />

Tangu kuingia kwake Madinah, Mtume (s.a.w) na Masahaba<br />

wake hawakupata amani angalau kwa mfululizo wa miezi<br />

michache. Wakati mwingine ilikuwa hapana mwezi unaopita bila<br />

ya kuwa katika mapigano ya vita na maadui wa Uislamu.<br />

Kukosekana kwa amani ilikuwa ni kikwazo kikubwa sana<br />

kwa kazi ya kuufikisha ujumbe wa Uislamu kwa watu. Katika<br />

mwezi wa Dhul-Qa’dah 6 A.H. akiwa na Waislamu 1400 Mtume<br />

(s.a.w) alifunga safari kuelekea Makkah kufanya U’mrah.<br />

Maquraish walipopata habari waliweka vizuizi katika njia<br />

zote za kuingilia Makkah kumzuia Mtume (s.a.w) na masahaba<br />

wasipenye kuingia Makkah. Mtume alilazimika kupiga kambi<br />

sehemu iitwayo Hudaibiya.<br />

Baada ya mjadala mrefu baina ya Waislamu na Maquraish,<br />

pande zote mbili ziliafikiana kuweka mkataba wa amani wa miaka<br />

kumi wenye masharti yafuatayo:<br />

(1) Waislamu watarudi Madinah bila kufanya Umrah.<br />

(2) Waislamu wanaweza kurudi mwakani (7:A.H.) kufanya<br />

Umrah lakini wakae siku tatu.<br />

(3) Wakija Makkah, wasije na silaha ila panga zikiwa ndani ya ala.<br />

(4) Waislamu hawataenda nao Madinah Waislamu wanaoishi<br />

Makkah na wala hawatamzuia yeyote miongoni mwao<br />

anayetaka kubakia Makkah.<br />

(5) Kama yeyote atatoroka kwenda Madinah kusilimu,<br />

Waislamu hawana budi kumrudisha (wasimpokee) lakini<br />

yeyote kutoka Madinah akitoroka kwenda Makkah<br />

Maquraish watampokea.<br />

181

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!