Download - islamic education panel
Download - islamic education panel
Download - islamic education panel
Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
Hivyo ndoa ya Mtume (s.a.w) na Bibi Khadija haikutokea<br />
kwa bahati nasibu tu, bali ulikuwa mpango madhubuti wa Allah<br />
(s.w) ili kumtajirisha Mtume ili aweze kutoa mchango wake katika<br />
kuwahurumia na kuwasaidia madhaifu katika jamii yake, na ili awe<br />
mfano wa kuigwa na matajiri katika kutoa mali kwa ajili ya Allah<br />
katika kuwahurumia wanajamii. Qur-an inatufahamisha:<br />
Na akakukuta fakiri akakutajirisha?” (93:8)<br />
Muhammad (s.a.w) alikuwa fakiri kabla ya kumuoa Khadija<br />
na kuwa tajiri mkubwa baada ya kumuoa Khadija<br />
(vi) Kuchukia maovu na kujitenga pangoni<br />
Kuchukia maovu na kujitenga pangoni, ni tukio lingine<br />
linaloonesha kuandaliwa kwa Mtume (s.a.w). Muhammad (s.a.w)<br />
tangu angali kijana alijihusisha mno na masuala ya kijamii na<br />
alikuwa akikereka sana kuona wanyonge wakidhulumiwa. Akiwa<br />
na umri wa miaka 20 alijiunga na Chama cha kuwatetea wanyonge<br />
dhidi ya Madhalimu. Mtume (s.a.w) alikosa usingizi kwa Sababu<br />
ya matatizo ya wengine na alikuwa na shauku kubwa ya kutafuta<br />
njia ya kuitoa jamii yake kwenye uovu na upotofu na kuipeleka<br />
kwenye wema na uongofu. Katika hali hiyo ilibidi ajitenge pangoni<br />
ili kutafuta msaada kwa Muumba Wake na aliupata kwa njia ya<br />
ndoto na baadaye kutumiwa Malaika Jibril. Allah (s.w)<br />
anamkumbusha Mtume wake juu ya maandalizi haya:<br />
“Je! Hatukukupanulia kifua chako. Na tukakuondolea<br />
mzigo wako (mzito) uliovunja mgongo wako?” (94:1-3)<br />
“Na akakukuta hujui kuongoza njia akakuongoza?” (93:7).<br />
47