08.06.2013 Views

Download - islamic education panel

Download - islamic education panel

Download - islamic education panel

SHOW MORE
SHOW LESS

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

Na kadhalika tulijaalia kila mji wakuu wao ndio waovu.<br />

Ikawa humo wanafanya hila (na vitimbi vya kuzuilia watu na<br />

dini ya Mwenyezi Mungu) wala hawafanyi hila isipokuwa<br />

nafsi zao lakini hawatambui. (6:123)<br />

Wakuu hawa waliochukua nafasi ya Allah (s.w) ya<br />

kuwatungia watu wa jamii zao sheria na mwongozo wa maisha,<br />

walijiweka juu ya jamii zao na kujihalalishia kuidhulumu jamii.<br />

Hofu kubwa ya wakuu hawa wa jamii za kikafiri na kishirikina ni<br />

kwamba, wakiuachia Uislamu ukisimama katika jamii, watakosa<br />

maslahi yao, kwani haki itasimama na hawatampata tena wa<br />

kumkandamiza wala kumnyonya. Hivyo hamu yao kubwa ni<br />

kuuzuia Uislamu usisimame katika jamii zao ili wawe na uhakika<br />

wa kuendeleza dhuluma bila ya kipingamizi. Allah (s.w)<br />

anatuhadharisha juu ya hila zao katika aya ifuatayo:<br />

............<br />

“…....... Wala hawataacha kupigana nanyi mpaka wakutoeni<br />

katika dini yenu kama wakiweza. Na watakaotoka katika<br />

dini yao katika nyinyi, kisha wakafa makafiri, basi hao ndio<br />

ambao amali zao zimeharibika katika dunia na akhera. Nao<br />

ndio watu wa Motoni, humo watakaa milele. (2:217)<br />

Hivyo Waislamu wanatakiwa watambue wazi kuwa makafiri<br />

na washirikina ni maadui zao na kamwe wasiwafanye wapenzi wao<br />

na marafiki zao kama Allah (s.w) anavyotutahadharisha:<br />

135

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!