Download - islamic education panel
Download - islamic education panel
Download - islamic education panel
Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
Hatutaweza kumuigiza Mtume(s.a.w) katika kusimamisha<br />
Uislamu bila ya kujiandaa kama yeye alivyoandaliwa na Mola wake<br />
au bila ya kuzingatia na kuyatia vitendoni mafunzo tunayopata<br />
kutokana na kuandaliwa kwake.<br />
Zama za Jahiliyyah<br />
Zama za jahiliyyah ni zile zama ambazo watu walikuwa<br />
wakiendesha maisha yao ya kibinafsi na kijamii kwa kufuata<br />
matashi yao kinyume na muongozo wa Allah(s.w.) na Mitume<br />
wake. Wakati Mtume (s.a.w) anazaliwa katika karne ya Sita (570<br />
A.D) dunia ilikuwa katika giza totoro la ujahili. Wakazi wa Bara<br />
Arab, katika kipindi hicho walikuwa chini sana kimaadili. Ubabe,<br />
unyanganyi na uporaji mali ya misafara ya biashara yalionekana<br />
matendo ya kishujaa na ya kujivunia. Wanyonge hawakuwa na<br />
haki, wanawake walinyanyaswa na kudhalilishwa hadi kufikia<br />
watoto wa kike kuzikwa wangali hai na wanawake kurithiwa kwa<br />
nguvu kama ilivyorithiwa mali.<br />
Kwa muhtasari hali ya Bara Arab wakati huo wa Jahiliya<br />
ilikuwa kama alivyoeleza Jaffari bin Abu Twalib mbele ya Mfalme<br />
Najash kwa niaba ya waislamu aliwaongoza katika hijira ya<br />
Uhabeshi:.<br />
“Ewe Mfalme, sisi tulikuwa waovu na majahili,<br />
tukiabudia masanamu na kula nyamafu hata mizoga ya<br />
wanyama waliokufa wenyewe.Tulifanya kila aina ya<br />
matendo machafu na ya aibu. Hatukuwa wenye<br />
kuwajibika kwa jirani na jamaa zetu. Wenye nguvu<br />
miongoni mwetu waliwakandamiza wanyonge. Kisha<br />
Allah akamleta Mtume miongoni mwetu ambaye<br />
tulimfahamu vema kwa nasaba yake, utukufu wake na<br />
uzuri wa tabia yake adhimu. Alituita tumuabudu Mungu<br />
mmoja tu na akatukataza kuabudia masanamu na mawe.<br />
Alitufundisha kusema ukweli kutunza amana,<br />
38