08.06.2013 Views

Download - islamic education panel

Download - islamic education panel

Download - islamic education panel

SHOW MORE
SHOW LESS

You also want an ePaper? Increase the reach of your titles

YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.

Makafiri ambao, wamekanusha kuwepo kwa Allah (s.w.),<br />

lengo hili la kuumbwa binaadamu hawalitambui na huishi hapa<br />

duniani kwa lengo tu la kustarehe. Hivyo, wale makafiri<br />

wanaoshika hatamu ya uongozi katika jamii, huwawekea raia wao<br />

kanuni na sheria zitakazowawezesha (watawala hao) kuishi kwa<br />

starehe bila ya kujali maslahi ya raia. Kwa hiyo, raia waumini chini<br />

ya utawala wa kitwaaghut (kikafiri) nao watalazimika kufuata<br />

kanuni na sheria za twaaghut zinazopingana na kanuni na sheria za<br />

Allah (s.w.) katika kuendea kila kipengele cha maisha ya kijamii,<br />

kama vile uchumi, siasa, utamaduni, n.k. Hivyo, waumini wa<br />

sampuli hii, hata kama watakuwa wanaswali, wanatoa zakat,<br />

wanafunga, wanahiji na kufanya Ibada nyingine kama hizi za<br />

kibinafsi, sehemu kubwa ya maisha yao watakuwa wanaishi nje ya<br />

lengo la kuumbwa kwao. Waumini wa sampuli hii, wanaoridhika<br />

kuishi chini ya utawala wa twaaghut, mbele ya Allah (s.w.) ni<br />

washirikina kama inavyobainika katika aya ifuatayo:-<br />

Wamewafanya wanavyuoni wao na watawa wao kuwa ni<br />

miungu badala ya Mwenyezi Mungu, na (wamemfanya) Masihi<br />

mwana wa Maryamu (pia Mungu) hali hawakuamrishwa<br />

isipokuwa kumuabudu Mungu mmoja, hakuna anayestahiki<br />

kuabudiwa ila Yeye. Ametakasika na yale wanayomshirikisha<br />

nayo. (9:31)<br />

Mayahudi na Wakristo, katika aya hii wanalaumiwa kuwa<br />

wamewafanya viongozi wao (Mapadre na Mafarisayo) kuwa<br />

miungu badala ya Allah (s.w.). Katika kuitafsiri aya hii Mtume<br />

(s.a.w.) aliwafahamisha waumini kuwa, kuwafanya viongozi<br />

miungu badala ya Allah (s.w.), ni pale viongozi watakapotiiwa na<br />

kufuatwa kinyume na sheria na mwongozo wa Allah (s.w).<br />

16

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!