08.06.2013 Views

Download - islamic education panel

Download - islamic education panel

Download - islamic education panel

SHOW MORE
SHOW LESS

You also want an ePaper? Increase the reach of your titles

YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.

(ii) Kutumia Lugha Nyepesi Inayofahamika<br />

kwa Wanafunzi.<br />

Mwalimu anapofundisha somo lolote lisilokuwa lugha, lengo<br />

lakesikufundishalugha inayotumika kufundishia bali lengo lake ni<br />

kumuwezesha mwanafunzi kubaini dhana (concepts) za mada<br />

husika. Hivyo ni wajibu wake kutumia lugha nyepesi na<br />

inayofahamika kwa wanafunzi wake.<br />

Ni katika maelekezo ya Allah (s.w) kuwa tunapofikisha<br />

ujumbe wa msingi kwa watu tuufikishe kwa lugha zao, kwani Yeye<br />

Mwenyewe (s.w) ndivyo anavyofanya katika kuwafikishia ujumbe<br />

Waja wake.<br />

“Na hatukumpeleka Mtume yeyote isipokuwa kwa lugha ya watu<br />

wake ili apate kuwabainishia. Kisha Mwenyezi Mungu<br />

anamuacha kupotea Amtakaye (kwa kuwa mwenyewe hataki<br />

kuongoka), na humuongoza Amtakaye. Naye ni Mwenye nguvu<br />

(na) Mwenye hikima” (14:4).<br />

Kwa mnasaba wa aya hii ni jambo la busara na hekima kwa<br />

hapa Tanzania kuwafundisha watu Maarifa ya Uislamu kwa<br />

Kiswahili au,kwa lugha ya kabila husika ikibidi, kuliko kutumia<br />

kiarabu au lugha nyingineyo ya kigeni isiyofahamika vyema kwa<br />

wanafunzi unaowafundisha.<br />

Ukirejea historia jamii yetu ya Waislamu kuwa hivi ilivyo,<br />

imechangiwa kwa kiasi kikubwa, kwa kutumia lugha ya<br />

kiarabu, isiyojulikana kwa watu, kuwa ndio lugha pekee ya<br />

kufundishia Uislamu. Mpaka hivi leo kuna baadhi ya Waislamu,<br />

tena wanachuoni, wanaoamini kwamba mtu hawezi kupata Elimu<br />

ya Mwongozo (Maarifa ya Uislamu) bila kutumia lugha ya kiarabu.<br />

213

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!